Posts

DKT. TAX APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI WA ZAMBIA, BRAZIL NA VATICAN

Image
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amepokea nakala za Hati za Utambulisho za mabalozi wateule wa nchi za Zambia, Brazil na Vatican. Mhe. Waziri Tax amepokea nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Zambia nchini, Mhe. Mathew Jere, Balozi mteule wa Brazil nchini, Mhe. Gustavo Martins Nogueira na Balozi Mteule wa Vatican Nchini, Mhe. Askofu Mkuu Angelo Accattino leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Akizungumza na mabalozi hao kwa nyakati tofauti Waziri Tax amewahakikishia ushirikiano kutoka Serikalini wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao ya kibalozi hapa nchini. Pia Waziri Tax ametoa rai kwa mabalozi hao kuendeleza na kudumisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na nchi zao. “Tanzania na Zambia tumekuwa marafiki na ndugu wa muda mrefu, Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Serikali ya Zambia katika sekta za biashara na uwekezaji kwa maslahi mapana ya pande zote mbili,” alisema Dkt. Tax   B

KAMISHNA WA POLISI SUZAN KAGANDA AONGOZA MAHAFALI KIDATO CHA SITA BARBRO JOHANSSON

Image
Kamishna wa Jeshi la Polisi nchini, Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, Suzan Kaganda, kimkabidhi cheti mwanafunzi bora wa masomo ya sayansi, Myla Matondane wakati wa mafahali ya wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya Wasichana ya Barbro Johansson, jijini Dar es Salaam Kamishna wa Jeshi la Polisi nchini, Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, Suzan Kaganda, aliyekuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya 17 ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita ya Shule ya Wasichana ya Barbro Johansson, akizungumza na wahitimu (hawapo pichani) wakati wa sherehe hizo, Jijini Dar es Salaam jana. Mwenyekiti Mwanzilishi wa Joha Trust, Profesa Anna Tibaijuka, akizungumza wakati wa sherehe za Mahafali ya 17 ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Wasichana ya Barbro Johansson, iliyopo Luguluni Wilaya ya Ubungo, Jijini Dar es Salaam Mkuu wa Shule ya Wasichana ya Barbro Johansson, Jospina Leonidace, akizungumza kuhusu historia ya shule katika Mahafali ya 17 ya Kidato cha Sita wakati wa sherehe hizo zilizof

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI

Image
 

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI FEB 26, 2023

Image
 

SERIKALI ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI-MAJALIWA

Image
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kushirikiana kikamilifu na Sekta Binafsi katika utoaji elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi ili kuzalisha wataalamu wenye ujuzi wa kutosha unaohitajika katika sekta mbalimbali. Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa waajiri wote nchini waendelee kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha malengo ya kukuza ujuzi na kuongeza soko la ajira yanafanikiwa kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa. Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Februari 24, 2023) katika hafla kati ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) na wadau kutambua mchango wa uzalishaji wa rasilimaliwatu yenye ubora kwa soko la ajira. ”Maendeleo ya uchumi wa nchi yoyote yanategemea sana ngazi ya ujuzi wa nguvukazi uliyokuwa nayo. Hivyo, mchango wa wadau ni muhimu.” Kadhalika, Waziri Mkuu amewapongeza waajiri kwa kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo (field practical), uanagenzi,  utarajali pamoja na namna wanavyoshiriki wenu katika k

HAKUNA MGONJWA ALIYEKUFA KWA KUTOKUWEKEWA "PACEMAKER"-JKCI

Image
Madaktari bingwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) Tulizo Shemu na Yona Gandye wakimwekea mgonjwa kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Pacemaker) tarehe 24/02/2023  

WAZIRI NCHEMBA AMPOKEA RAIS WA BENKI YA MAENDELEO BARANI AFRIKA AFDB

Image
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili nchini katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, kwa ziara ya kikazi.  Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, (Mb), akiteta jambo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, AfDB,  Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili nchini katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, kwa ziara ya kikazi.     Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), mwenye skafu ya Bendera ya Taifa, akiwa katika picha na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB),  Dkt. Akinwumi Adesina ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi, pamoja na ujumbe kutoka AfDB na Tanzania, baada ya kuwasili , jijini Dar es Salaam. 

JK AMSHUKURU RAIS MSTAAFU BUSH KWA KUANZISHA MPANGO WA PEPFAR KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA

Image
  WASHINGTON DC. Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  amemshukuru Rais Mstaafu wa Marekani George W. Bush kwa uamuzi alioufanya kusaidia mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kuanzisha mpango wa Dharura wa Rais wa kupambana na UKIMWI PEPFAR ambapo serikali ya Marekani hutoa fedha za kununua dawa (ARVs) za kufubaza vijidudu vinavyosababisha maambukizi ya UKIMWI kwa watu walioathirika. Dkt. Kikwete amesema mpango huo umeokoa maisha ya mamilioni ya binadamu ambapo kwa sasa UKIMWI sio "adhabu ya kifo". Dkt. Kikwete ambaye alialikwa na muasisi wa mpango huo, Rais Mstaafu wa Marekani George W. Bush,  katika kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwa mpango huo jijini Washington DC. Ijumaa, Feb. 24, 2023 . PEPFAR ILIVYOANZISHWA Wakati Rais Bush anatangaza PEPFAR mwaka 2003, kwa uchache watu 50,000 chini ya jangwa la Sahara ndio Walikuwa na fursa ya kupata ARVs. Leo hii inakadiriwa mpango wa PEPFAR ambao unaendelea kutekelezwa katika Nchi zaidi ya 50 umeokoa maisha ya watu milioni 2