Posts

JNHPP KUONDOA CHANGAMOTO ZA UPUNGUFU WA UMEME- EWURA

Image
  Na Mwandishi Wetu Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesema kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP)  linalojengwa Rufiji mkoani Pwani litaondoa changamoto za upungufu wa umeme nchini na mradi huo unategemewa kuzalisha megawati 2115 pindi utakapokamilika Juni 2024. Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya siku moja katika mradi huu, Mwenyekiti wa Bodi hiyo Profesa  Mark Mwandosya amesema, mradi wa JNHPP ni wa kisasa kwa sababu ni mradi mkubwa  ukilinganisha na miradi mingine ambayo imeshajengwa lakini pia utazalisha umeme kwa kiwango kikubwa na utawezesha watanzania kupata umeme wa uhakika. “Kama nilivyosema uzalishaji wa umeme utakuwa mkubwa kwa hiyo kwa miaka mingi sitegemei kwamba tutakuwa na uhaba wa upatikanaji wa umeme. Umeme ni mfumo lakini pia mambo mengine yanayoambatana na nayo ni njia za kusambaza umeme, njia za kupeleka umeme kwenye vyanzo. "Sasa lazima kila wakati kuwe

KATIBU MKUU JUMUIYA YA WAZAZI : WAZAZI TUJIKITE KUTOA ELIMU YA MAADILI KWA JAMII

Image
  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Gilbert Kalima akizungumza  na wananchi, Wana CCM na viongozi wa chama hicho wa Wilaya ya Singida katika mkutano uliofanyika Ofisi ya CCM  Mkoa wa Singida ikiwa ni moja ya matukio katika mfululizo wa ziara yake. Na Dotto Mwaibale , Singida KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Gilbert Kalima, ametoa rai kwa wazazi kujikita katika jukumu la kutoa elimu kwa jamii kuhusu suala la maadili kutokana  na hivi sasa kuanza kujitokeza mfululizo wa matukio ya unyanyasaji wa kijinsia hapa nchini. Akizungumza leo na wananchi,wanachama na viongozi wa CCM Wilaya ya Singida, amesema suala la malezi ya watoto ni jukumu la Jumuiya ya Wazazi kwani hivi sasa kumeanza kujitokeza mwenendo usiofaa kwa jamii katika nchi yetu. "Kila tukikaa ndani ya siku mbili ukisikiliza vyombo vya habari wanakwambia kuna unyanyasaji wa kijinsia, mara utasikia baba kamuua mama,mara mama kauawa na mtoto au mama kaua mtot

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI JANUARI 29, 2023

Image
 

WAZIRI MKUU AWASISITIZA WABUNGE WASHIRIKI MICHEZO

Image
 DODOMA WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa leo Jumamosi, Januari 28, 2023 ameshiriki Bunge Bonanza lililofanyika katika viwanja vya shule ya msingi na sekondari ya John Merlin ya jijini Dodoma ambapo ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wabunge na wananchi wengine washiriki katika michezo ili kuipa miili yao nguvu na uwezo wa kutekeleza majukumu yao ya kikazi. “…Michezo kwetu sisi wabunge ni muhimu zaidi kwa sababu inatufanya tuwe na afya bora zaidi na pia michezo inasaidia watu kukutana pamoja na kuimarisha undugu, kujenga urafiki pamoja na kukuza vipaji. Nampongeza Mheshimiwa Spika Dkt. Tulia Ackson kwa ubunifu huu wa kuanzisha Bunge Bonanza ambalo litakuwa linafanyika mara kwa mara.” Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo wakati akizungumza na wabunge, baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Watumishi wa Bunge pamoja na maafisa wengine wa Serikali walio shiriki katika bonanza hilo. Amesema bonanza lingine kama hilo linatarajiwa kufanyika Juni 24, 2023. Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Dkt. Tul

RAIS SAMIA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI WA KAMPUNI YA MAFUTA YA ENOC LLC YA UAE.

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Taifa ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ENOC LLC, Bw. Saif Al Falasi aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Januari, 2023.  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Nishati tarehe 27 Januari, 2023 walisaini Mkataba wa makubaliano (Memorandum of Understanding) na Kampuni hiyo ya ENOC LLC kuhusu Ujenzi wa Kitovu cha Mafuta (Fuel Hub) hapa nchini  

VIONGOZI WA DINI, WAZEE WAUPA BARAKA MSWADA WA BIMA YA AFYA KWA WOTE.

Image
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu ameendelea na vikao vyake vya kukutana na makundi mbalimbali vyenye lengo la kutoka elimu kuhusu Bima ya Afya kwa Wote. Safari hii Mhe. Waziri Ummy amekutana na viongozi wa dini na Wazee. "Lengo likiwa ni kutoa Elimu na kupokea maoni yao kuhusu Mswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote." amesema Mhe. Ummy na kuongeza...Tunawashukurusana viongozi wetu kwa kuunga mkono mswada huu na kutupa baraka tusonge mbele kwa kutambua kuwa Afya ndio kila kitu.