Posts

PSSSF KATIKA MAONESHO YA BIASHARA NA UTALII TANGA

Image
 NA MWANDISHI WETU, TANGA   MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unashiriki katika maonesho ya bishara na utalii kwa kutoa elimu kwa wanachama kupitia maonesho yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako jijini Tanga. PSSSF   inashiriki katika maonesho haya pamoja na kutoa elimu kwa wanachama na wananchi wanaotembelea banda hilo, pia wanachama wanapatiwa huduma mbalimbali za kiofisi ikiwemo,   kuangalia taarifa za michango ya wanachama,   taarifa za malipo ya pensheni, uhakiki wa wanachama na kutoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya uanachama, alisema Bi. Rehema Mkamba, Afisa Mkuu wa Uhusiano, PSSSF Alisema ni fursa nzuri kwa Mfuko kukutana na wanachama wake lakini wananchi pia ambao watafika kwenye maonesho hayo  maarufu kama Tanga Trade Fair  ambayo yatadumu kwa siku 10 kuanzia Mei 28   hadi Juni 6, 2022. Wanachama wa PSSSF wakihidumiwa kwenye banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya biashara na utalii kwenye viwanja vya Mwahako jijini Tanga. Wananchi na wanachma

WANAFUNZI WA VYUO WAFURAHIA KUJIUNGA NA NSSF, WENYEWE WASEMA NI FURSA KWAO YA KUJIWEKEA AKIBA.

Image
  NA MWANDISHI WETU, MOROGORO WANAFUNZI wa Chuo cha Mzumbe na Chuo cha Jordan  Mkoani Morogoro wamehamasika kujiunga na Mfuko wa NSSF kupitia Mpango wa Taifa  wa Sekta Isiyo Rasmi chini ya kampeni ya “Boom Vibes na NSSF” iliyotua mkoani Morogoro Mei 28, 2022. Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanachuo hao,  Meneja wa Sekta Isiyo Rasmi, Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bi. Rehema Chuma amewahakikishia kuwa hawatajutia uamuzi wa kujiunga na Mfuko huo kwani utawasaidia katika maisha yao ya sasa na baadaye. “Ni muhimu wewe kama mwanachuo kuanza utamaduni wa kujiwekea akiba kupitia NSSF, ukianza kuweka akiba mapema itakuwezesha kuwa na akiba ya kutosha inayoweza kuwa mtaji wa biashara pindi utakapomaliza elimu yako.” Alisema unapokuwa mwanachama wa NSSF unatakiwa kuhakikisha unachangia kiasi kisichopungua shilingi elfu ishirini (20,000/=) kila mwezi au zaidi na uwasilishaji michango ni rahisi kupitia mitandao ya simu na benki. Alisema Hifadhi ya Jamii ipo makhususi kwa ajili ya k

"BOOM VIBES NA NSSF" MATUKIO KATIKA PICHA IFM NA CHUO CHA KUMBUKUMBU YAMWALIMU NYERERE

Image
  NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, IFM Kampeni ya uhamasishaji wa hifadhi ya jamii na uwekaji akiba kwa wanachuo inayokwenda kwa jina la “Boom Vibes na NSSF” imetua chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es Salaam ambapo mamia ya wanachuo wamejiunga na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu kwa wanachuo kuhusu umuhimu wa Hifadhi ya Jamii na uwekaji wa akiba katika Mfuko kupitia Mpango wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi ili wanachuo wajenge tabia ya kuweka akiba kwa manufaa ya sasa na baadaye kwa kujiandikisha na NSSF na kuchangia kila mwezi ambapo kima cha chini ni shilingi elfu 20,000/=, Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma, NSSF, Bi. Lulu Mengele amesema. Bi. Lulu Mengele ambaye alifuatana na Meneja wa NSSF Mkoa wa Temeke Bw. Feruzi Mtika, alisema Mei 28, 2022, kampeni hiyo ilifanyika kwenye vyuo vingine vitatu, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Kigamboni jijini Dar es Salaam, Chuo cha Mzumbe na Chuo cha Jordan vyote

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI MEI 29, 2022

Image