Posts

PROF. MBARAWA ATOA MIEZI MITATU UKARABATI MV. KAZI

Image
  WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amemtaka mkandarasi Songoro Marine anayefanya ukarabati mkubwa wa Kivuko cha MV. Kazi kuhakikisha kivuko hicho kinakamilika ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia sasa. Akizungumza alipokagua ukarabati wa kivuko hicho leo jijini Dar es Salaam, Prof. Mbarawa amesema Serikali imeshapata fedha kwa ajili ya ukarabati huo, hivyo ni wajibu wa Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) na Mkandarasi Songoro Marine kuhakikisha taratibu za manunuzi na mikataba ya kazi hiyo inakamilika kwa haraka. "...Hakikisheni ifikapo Ijumaa ya Aprili Mosi taratibu za mikataba ziwe zimekamilika na kasi ya ujenzi na uagizaji vifaa nje ya nchi kwa ajili ya kazi hiyo iongezeke ili kufikia lengo," amesisitiza Prof. Mbarawa.   Prof. Mbarawa amesema idadi ya wakazi wa Kigamboni wanaohitaji huduma ya kivuko imekuwa ikiongezeka siku hadi siku hivyo kuwataka TEMESA kutengeneza ratiba maalum ya ukarabati wa vivuko vyake ili kuondoa usumbufu pindi v

TANZANIA NA ISRAEL KUSHIRIKIANA KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA MAGONJWA YA MOYO KWA WATOTO

Image
 Na Catherine Sungura, WAF-Dodoma Tanzania na Israel  kushirikiana katika kuboresha huduma za Magonjwa ya moyo kwa watoto kupitia Shirika  la SACH linalojishughulisha na huduma za magonjwa hayo kwa watoto nchini humo. Akiongea wakati wa kikao hicho leo kilichofanyika jijini Dodoma kati ya Wizara ya afya na Mtendaji Mkuu wa Shirika la huduma za magonjwa ya moyo kwa watoto (Save a Child’s Heart - SACH Bw. Simon Fisher, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi amesema kuwa wamekubaliana kuendeleza ushirikiano katika masuala yanayohusiana na huduma hizo hapa nchini. “Kikao hiki kilikua na lengo la kujadiliana maeneo ambayo Wizara ya Afya inaweza kushirikiana na shirika la SACH katika kuongeza idadi ya wataalam watakaopata mafunzo ya muda mfupi na ya muda mrefu nchini Israel katika Ubingwa na Ubingwa bobezi wa magonjwa ya moyo kwa watoto”. Aidha, Prof. Makubi amemshukuru Mkurugenzi huyo kwa kutoa huduma za moyo kwa watoto kupitia kambi za matibabu hapa nchini kuanzia mwaka 2015. Prof

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI WORLD GOVERNMENT SUMMIT DUBAI MACHI 29

Image
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango leo tarehe 29 Machi 2022 ameshiriki ufunguzi wa Jukwaa la 8 la Wakuu wa Nchi na Serikali Duniani linalofanyika Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu. Makamu wa Rais anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika jukwaa hilo ambapo Pamoja na mambo mengine lina lengo la kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na kubadilishana mbinu za kuimarisha utendaji wa serikali Katika Ufunguzi wa Jukwaa hilo viongozi wakuu wa serikali, mashirika ya kimataifa pamoja na sekta binafsi kutoka nchi mbalimbali wamekutana na kujadili namna bora ya kuongeza ufanisi katika utoaji huduma za serikali kwa wananchi na kutatua changamoto mbalimbali kupitia utafiti kwa kuzingatia mabadiliko yanayoendelea duniani Hapo kesho tarehe 30 Machi 2022 Makamu wa Rais Dkt. Mpango anatarajiwa kuzungumza katika jukwaa hilo akichangia mada ya “kwanini Afrika imekua ni muhimu sana kwa wakati huu katika uchumi wa

Benki Ya CRDB Yasaini Mkataba Wenye Thamani Ya Sh. Bilioni 182 Na Proparco Kuwezesha Wajasiriamali Nchini

Image
 Benki ya CRDB imeingia makubaliano ya uwezeshaji wajasiriamali wadogo na wakati (MSMEs) wenye thamani ya Shilingi bilioni182 na shirika la fedha la nchini Ufaransa la Proparco. Makubaliano hayo ambayo yanajumuisha mkopo na dhamana za mikopo kwa wajasiriamali, itasaidia kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na mpango wa maendeleo wa Taifa, kwa kuzingatia zaidi wajasiriamali wanawake, wajasiriamali katika sekta ya kilimo, pamoja na wajasiriamali ambao wameathirika kwa kiasi kikubwa na janga la UVIKO-19.  Proparco, ni kampuni tanzu ya shirika la maendeleo la UfaransaAgence Française de Développement Group (AFD Group), ambalo limejikita katika kutoa ufadhili na usaidizi kwa biashara na taasisi za kifedha barani Afrika, Asia, Amerika Kusini na Mashariki ya Kati.  Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano hayo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema ushirikiano huo umekuja wakati muafaka na utasaidia kwa kiasi kikubwa ku

RAIS SAMIA AKUTANA NA MKURUGENZI WA OPEC FUND DKT. ALKHALIFA ABDULHAMID

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Nchi zinazozalisha Mafuta kwa wingi Duniani (OPEC Fund) Dkt. Alkhalifa Abdulhamid Saleh, Ikulu Chamwino leo tarehe 29 Machi, 2022.  

DRC YAJIUNGA RASMI JUMUIYA YA AFRIKA MADHARIKI

Image
  MKUTANO wa Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)  uliyofanyika kwa njia ya mtandao na kuongozwa na Mwenyekiti wake Rais Uhuru- Kenyatta wa Kenya, umeridhia kwa kauli moja Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kuwa mwanachama wa Jumuiya hiyo. Kujiunga kwa DRC kwenye jumuiya hiyo, kunafanya idadi ya Wanachama kuwa nchi 7, nchi zingine no Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini. Wachambuzi wa masuala ya siasa na uchumi wanasema kujiunga kwa DRC) kwenye jumuiya kunafanya EAC kuwa na Watu karibu milioni 280 na Uchumi wenye GDP ya USD bilioni 262. Kenya inaongoza kwa Uchumi mkubwa wa USD 95.5bn, ikifuatiwa na Tanzania USD 63.2bn na ya Tatu ni DRC USD 50.4bn.

ZAIDI YA WANANCHI 22,000 WA NYANGAO - MTAMA KUPATA MAJI SAFI NA SALAMA

Image
 Mbunge wa Jimbo la Mtama na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye ameshuhudia utiaji saini wa mkataba baina ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa Mkoa wa Lindi na mkandarasi wa Kampuni ya Halem Construction Limited kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji safi na salama wa mradi wa Nnyangao - Mtama  Ujenzi wa mradi huo utanufainisha na kuwawezesha wananchi zaidi ya 22,000 kupata maji safi na salama ambao utagharimu zaidi ya shilingi 4,577,244,446 Mradi huo utatekelezwa jimboni humo  kwenye kata tatu za Majengo, Mtama na Nyangao zenye jumla ya vijiji 13    vya Nyangao A,  Nyangao B, Mtakuja II, Nangaka, Masasi, Majengo A, Majengo B, Mvuleni, Mihogoni, Mbalala, Makonde, Mnamba (Chluwe) na Mkwajuni Viongozi wengine walioambatana na Mhe. Waziri Nape  ni Mhe. Shaibu Issa Ndemanga, Mkuu wa Wilaya Lindi; Mhe. Yusuph Abdalah Tipu, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mtama; Waheshimiwa madiwani wa maeneo husika, watendaji wa Ruwasa na Viongoz

TANZANIA, LIECHTENSTEIN KUWEKEZA KATIKA KILIMO HAI

Image
  Na Mwandishi wetu, Dar Tanzania na Liechtenstein zimekubaliana kuweka mpango mkakati wa kuwekeza katika kilimo hai na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo katika mikoa ya Morogogo na Dodoma. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Liechtenstein Mhe. Dominique Hasler ambaye yuko nchi kwa ziara ya kikazi. Katika mazungumzo hayo viongozi hao wamekubalia kuangazia maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za Utalii, Viwanda, na Elimu, hususan kumuendeleza mtoto wa kike katika masomo ya sayansi na teknolojia. “Tumekubaliana mara baada ya ziara yake tuweze kuangazia namna gani tunaweza kudumisha na kuendeleza maeneo mapya ya ushirikiano baina yetu kwa maslahi ya Tanzania na Liechtenstein,” Amesema balozi Mulamula. Nae Waziri wa Mambo ya Nje wa Liechtenstein Mhe. Dominique Hasler amesema Liechtenstein ina uhusiano imara na wa siku nyingi, na tumeku

MTANZANIA ANAYEISHI NCHINI CANADA AONESHA NIA YA KUWEKEZA NCHINI KATIKA SEKTA YA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Image
Mtanzania anayeishi nchini Canada Bw. Joseph Katallah ameonesha nia ya kuja kuwekeza nchini katika sekta ya miundombinu kwa kushirikiana na kampuni ya Geopolymer Solutions LLC ya nchini Marekani hususan kwenye ujenzi wa barabara za lami kwa kutumia teknolojia mpya iliyogunduliwa na kampuni hiyo. Wawekezaji hao wanaoratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wapo nchini kwa ziara ya wiki moja ambapo wanatumia fursa hiyo kukutana na wataalamu wa sekta ya barabara kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini Tanzania - TARURA, Wakala wa Barabara Tanzania - TANROADS, na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Lengo la ziara ya wawekezaji hao pamoja na mambo mengine ni kuitangaza teknolojia mpya ya utengenezaji wa barabara za lami zisizotumia saruji ya kiwandani na badala yake zitatumia udongo mwekundu ambao pia unapatikana nchini. Wawekezaji hao wameeleza kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kupewa kip

MHE. JENISTA AWATAKA TAKUKURU KUISHI MAONO YA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN YA KUHAKIKISHA MIPANGO NA HUDUMA ZA MAENDELEO ZINAWAFIKIA WANANCHI KWA UKAMILIFU

Image
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma Tarehe 28 Machi, 2022 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ameielekeza Menejimenti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuhakikisha wanayaishi maono ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mipango na huduma za maendeleo zinawafikia wananchi kwa ukamilifu. Mhe. Jenista amesema hayo leo jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na Menejimenti ya TAKUKURU alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa taasisi hiyo. Mhe. Jenista amesema, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali anayoiongoza ya Awamu ya Sita imejipanga kikamilifu kuleta mageuzi makubwa kwenye taifa katika sekta zote ili wananchi wapate huduma bora na kwa wakati, hivyo, TAKUKURU wanao wajibu wa kuhakikisha maono ya Mhe. Rais pamoja na Serikali ya Awamu ya Sita yanafikiwa kwa ukamilifu. “TAKUKURU tuna deni kubwa sana kwa Watanzania katika kuhakikisha mipango na huduma zinazo