Posts

WIZARA YAONGEZA NGUVU KUDHIBITI UTOROSHAJI MAZAO YA UVUVI

Image
    Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi Bw. Emmanuel Bulayi (kushoto), akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (katikati) juu ya utendaji kazi wa injini tano za kupachika kwenye boti zilizonunuliwa na idara hiyo kwa ajili ya vituo vya ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi Kanda ya Ziwa Victoria. Hafla hiyo fupi imefanyika katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Aliye upande wa kushoto kwa katibu mkuu ni Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbemaji Dkt. Nazael Madalla. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Wizara ya Mifugo na Uvuvi). Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (kulia) akimkabidhi injini ya kupachika kwenye boti Afisa Mfawidhi Kituo cha Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Kanda ya Mwanza Bw. Gabriel Mageni na kuwataka maafisa wafawidhi kuhakikisha wanatumia vifaa hivyo kwa ajili ya kudhibiti utoroshaji wa mazao ya uvuvi kwenda nchi za j

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA OKTOBA 29, 2021

Image
 

WATAALAM MIPANGOMIJI WATAKIWA KUTENGA MAENEO YA WAFANYABIASHARA

Image
  Na   Munir Shemweta, WANMM MOROGORO Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Wataalam wa Mipangomiji nchini kuhakikisha wanapopanga mipango yao kwenye maeneo mbalimbali nchini wanatenga maeneo ya wafanyabiashara wa kawaida ili waweze kufanya biashara katika mazingira rafiki na yaliyo bora. Alisema, baada ya Wataalam hao kutekeleza wajibu wao wa kupanga, halmashauri nchini ambazo ni mamlaka za upangaji ziweke miundombinu ili wafanyanyabiashara hao wapatikane kwenye maeneo maalum yaliyotengwa. Kwa mujibu wa Dkt Mabula, maeneo yatakayotengwa kwa ajili ya wafanyabiashara wa kawaida ni sharti yawe na huduma zote muhimu kama vile maji, umeme na barabara ili kuwawezesha kufanya biashara zao hata usiku kwenye maeneo maalum yaliyotengwa. ‘’Mnapoandaa michoro yenu ya mipangomiji zingatieni taaluma huku mkikumbuka kuna makundi maalum kama vile Mamalishe, Machinga, Bodaboda na watanzania wa kawaida na muwawekee utaratibu maalum wa kupata ardhi kwa gharama

TMA: KUNA VIASHIRIA VYA UPUNGUFU WA MVUA MAENEO YANAYOPATA MVUA KWA MSIMU MMOJA

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utabiri wa muelekeo wa mvua za msimu, mwezi Novemba 2021 hadi Aprili 2022, leo Oktoba 27,2021 jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri Mamlaka ya Hali ya Hewa TMA, Dkt. Hamza Kabelwa.   Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi akizungumza na waandishi wakati wa utabiri wa muelekeo wa mvua za msimu mwezi Novemba 2021 hadi Aprili 2022, leo Oktoba 27,2021 jijini Dar es Salaam. MAMLAKA ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) imesema Upungufu wa Mvua unatarajiwa kujitokeza kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa Mvua kwa mwaka unaoanza mwezi Novemba 2021 hadi Aprili 2022. Imeelezwa kuwa mvua hizo zinatarajiwa kuwa chache yaani za chini ya wastani hadi wastani katika maeneo mengi ya mikoa ya kigoma, Tabora, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe, Mbeya na Iringa huku kwa mikoa ya Njombe, Ruvuma, Lindi, Mtwara na kusini mwa mk

RAIS SAMIA "AMWAGA " VIWANJA VYA KUJENGA NYUMBA KWA TWIGA STARS, NI ZAWADI BAADA YA KUTWAA KOMBE

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika Picha ya pamoja na Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Wanawake Twiga Stars mara baada ya kupokea Kombe la Ubingwa wa Cosafa kutoka kwa Wachezajia wa Timu ya hiyo leo tarehe 27 Oktoba, 2021 Ikulu Jijini Dar es Salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Viongozi na Wachezaji wa Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya  Wanawake Twiga Stars mara baada ya kupokea Kombe la Ubingwa wa Cosafa kwa Timu  hiyo leo tarehe 27 Oktoba, 2021 Ikulu Jijini Dar es Salaam. RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewapatia viwanja vya kujenga nyumba wachezaji wote wa timu ya Taifa ya Soka ya Wasichana Twiga Stars ikiwa ni zawadi yake kwa wachezaji hao baada ya kutwaa kombe la COSAFA 2021 linaloandaliwa na Baraza la Soka la Nchi za Kusini mwa Afrika. Rais pia amewapa zawadi za fedha wachezaji wote wa timu hiyo na benchi la ufundi kwa mafanikio hayo. Rais ametoa zawadi

WAZIRI BASHUNGWA AMUELEZA RAIS SAMIA MAFANIKIO SEKTA YA MICHEZO, SANAA NA UTAMADUNI

Image
  Na  John Mapepele, WUSM  Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent Bashungwa ameomba mashindano ya Kombe la Taifa, (Taifa CUP) yaliyorejeshwa na Wizara yake mwaka huu kuitwa Kombe la Taifa la Mama Samia (Samia Taifa CUP) kutokana na uzito wa mashindano hayo na nia njema ya Mhe, Rais ya kuendelea michezo nchini.  Mhe. Bashungwa ameyasema hayo leo Oktoba 27, 2021 kwenye hafla ya kupongeza timu ya soka ya Taifa ya Wanawake (Taifa Stars) iliyoandaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan jijini Dar es Salaam alipokuwa akifafanua  mafanikio ya Sekta za Utamaduni, Sanaa na Michezo katika kipindi hiki. Akielezea mafanikio hayo amesema kuwa ni pamoja na kuandaa mkakati pamoja  baina ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Baraza la Michezo la Majeshi Tanzania (BAMMATA) na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kwenye mashindano ya kimataifa na kuongeza kuwa wachezaji  46 wanacheza michezo ya kulipwa nje ya nchi.  Kuhusu maelekezo ya Mhe. Rais ya kuw

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI OKTOBA 28, 2021

Image