Posts

WAZIRI NDAKI ANG’AKA UKUSANYAJI MDOGO WA MADUHULI

Image
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) akizungumza wakati wa kupokea taarifa ya ukusanyaji wa maduhuli ya robo mwaka kwa bajeti ya wizara ya mwaka wa fedha 2021/22 Sekta ya Mifugo jijini Dodoma, ambapo Waziri Ndaki amesema utaratibu wa ukusanyaji maduhuli uko wazi lakini kuna shida ya namna ya ukusanyaji pamoja na fedha nyingine kutojulikana zinapopelekwa baada ya kukusanywa. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Wizara ya Mifugo na Uvuvi). Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akizungumzia kukerwa na utoroshaji wa rasilimali za mifugo nchini kwenda nje ya nchi na uingizaji wa mazao ya mifugo kinyume na utaratibu ambapo wanaweza kuwa wanaingiza mazao mbalimbali kwa kuwa hawalipi kodi na kuathiri uzalishaji ndani ya nchi mambo ambayo hayavumiliki. Amezungumza hayo wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya ukusanyaji wa maduhuli ya robo mwaka kwa bajeti ya wizara ya mwaka wa fedha 2021/22 Sekta ya Mifugo jijini Dodoma. (Picha na Kitengo cha Mawasil

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO OKTOBA 27, 2021

Image
 

UJERUMANI YATIA MGUU KUMPIGA JEKI RAIS SAMIA KIMAENDELEO

Image
  Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam UJERUMANI imeipatia Tanzania msaada wa Euro milioni 71, sawa na takribani shilingi za Tanzania bilioni 190.5 kwa ajili ya kutekeleza miradi kadhaa ikiwemo maji, uendelezaji wa maliasili na utalii, afya ya mama na mtoto pamoja na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia. Nyaraka za makubaliano ya msaada huo zimetiwa saini jijini Dar es Salaam kati ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayesimamia masuala ya Fedha za Nje Bi. Amina Khamis Shaaban na Kiongozi wa Ujumbe wa Serikali ya Ujerumani Bw. Marcus Von Essen. Akizungumza baada ya kutiwa saini kwa nyaraka hizo, Naibu Katibu Mkuu Bi. Amina Khamis Shaaban aliyataja maeneo yatakayonufaika na msaada huo kuwa ni afya ya mama na mtoto iliyotengewa Euro milioni 24 na mradi wa kuzuia migogoro baina ya wanyamapori na binadamu, utakao tumia Euro milioni 6. “Maeneo mengine yatakayonufaika na fedha hizi ni mpango wa kufidia upotevu wa makusanyo ya maduhuli katika sekta ya utalii kutokana na upungufu wa

PSSSF YAPOKEA GAWIO LA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7.6. KUTOKA BENKI YA CRDB

Image
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (watatu kushoto) akikabidhi mfano wa Hundi ya thamani ya shilingi bilioni 7.6 kama gawio kutoka benki ya CRDB kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), C.P.A. Hosea Kashimba (wanne kushoto) aliyeongozana na Mkurugenzi wa Fedha Beatrice Musa-Lupi (wapili kushoto) na Maafisa Uhusiano waandamizi wa Mfuko, Coleta Mnyamani (watano kushoto) na Fatma Elhady (Wasita kushoto) huku Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya benki ya CRDB, Ally Hussein Laay 9Wakwanza kulia) na wakwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Abdulmajib Nsekela. • Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba azipongez Taasisi za Umma kwa uwekezaji wa hisa kwenye benki. • Asema huo ndio utaratibu wa kuendesha uchumi kwa njia za kisasa. NA MWANIDHI WETU MFUKO wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umepokea gawio la zaidi ya shilingi bilioni 7.6 kutokana na uwekezaji wa hisa katika benki ya CRDB. Hafla ya kukabidhi GAWIO kwa

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE OKTOBA 26, 2021

Image