Posts

DC MOYO:WAKURUGENZI WATAKAOKAIDI MAAGIZO YA LISHE KUCHUKULIWA HATU KALI ZA KIDHAMU.

Image
  Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akizungumza kwenye kikao kazi na wanawake vinara wa lishe bora namna ya kutafuta njia ya kutatua tatizo la udumavu mkoani Iringa Baadhi ya wanawake vinara wa lishe bora wakiwa makini kumsikiliza meneja wa shirika lisilo la kiserikali la Save the Chidren mkoani Iringa John Masenza wakati semina ya kukabiliana na udumavu  mkoani Iringa. Na Fredy Mgunda,Iringa. Mkoa wa Iringa umeziagiza halmashauri zote kuhakikisha zinatenga na kutoa fedha kwa ajili ya kupambana na tatizo la udumavu ambalo limekuwa linaleta doa licha ya mkoa huo kuwa mmoja ya mikoa ambayo inaongoza kwa kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula. Akizungumza kwenye mkutano na wanawake vinara wa halmashauri tatu za mkoa huo,mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Iringa alisema kuwa kumekuwa na changamoto ya utolewa wa fedha kutoka kwa wakuu wa Idara mbalimbali za Halmashauri na kukwamisha mpango wa serikali ya mkoa kukabiliana natatizo la udum

WANAMUZIKI WAANZA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA SIKU YAO KIMATAIFA

Image
  Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania  (TAMUFO) Stella Joel. Stara Thomas Komandoo Hamza Kalala. Mwanamziki Mabisa.  Na Dotto Mwaibale  WANAMUZIKI Nchini wameanza maandalizi kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Muziki Duniani yatakayoadhimishwa kitaifa jijini Arusha. Akizungumza na waandishi wa jana Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania  (TAMUFO) Stella Joel alisema tayari wameanza kuandaa maandalizi kwa ajili ya maadhimisho hayo. "Tumeanza maandalizi ya Siku hiyo na tayari baadhi ya wanamuziki wamekwisha thibitisha kushiriki,". alisema Joel. Alisema kuwa leo saa 4 asubuhi katika Hoteli ya Kibo Palace Jijini Arusha watakutana  na waandishi wa habari na kuzungumzia kwa kina maandalizi hayo.  Joel aliwataja baadhi ya wanamuziki waliothibitisha kushiriki maadhimisho hayo  kuwa ni Komandoo Hamza Kalala, Stara Thomas na wengine wengi. Alisema kilele cha maadhimisho hayo itakuwa ni  Oktoba 1,2021.

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA AGOSTI 27, 2021

Image
 

SWEDEN YAIPATIA TANZANIA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 118 KUNUSURU KAYA MASIKINI

Image
  Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam Serikali ya Sweden imeipatia Tanzania msaada wa sarafu ya nchi hiyo (SEK) milioni 450 sawa na shilingi bilioni 118 za kitanzania kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini Awamu ya Pili kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF. Hati za makubaliano ya msaada huo zimetiwa saini Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Bw. Emmanuel Tutuba na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mheshimiwa Anders Sjöberg. “Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini Awamu ya Pili ulianza kutekelezwa mwaka 2020 na unatarajiwa kukamilika mwaka 2023, umepangiwa kutekelezwa kwa gharama ya dola za Marekani milioni 883.3 sawa na shilingi trilioni 2.02 na Sweden imesaidia jumla ya dola na Marekani milioni 237 sawa na shilingi bilioni 542.2” alisema Bw. Tutuba. Alisema kuwa mradi huo umelenga kuongeza fursa za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa pamoja na kulinda na kuimarisha rasilimali watu kwa kutoa ruzuku kwa

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI AGOSTI 26, 2021

Image
 

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 25, 2021

Image