Posts

WILAYA YA MANYONI YAZINDUA TASAF AWAMU YA TATU SEHEMU YA PILI

Image
  Mwakilishi wa Mkurugenzi wa  Mfuko wa Maendeleo wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) kutoka Makao Makuu,, Peter Lwanda akisoma taarifa ya TASAF Awamu ya Tatu Sehemu ya  Pili wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jwilayani humo mkoani Singida jana.. Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Rahabu Mwagisa, akizungumza katika uzinduzi huo. Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Manyoni, Jumanne Mgalaza, akitoa mkazo kkwa Madiwani kwenda  kuhakikisha walengwa ndio wanaonufaika na mpango huo. Wakuu wa Vitengo Ngazi ya Halmashauri na wa idara wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wilaya na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa  Mfuko wa Maendeleo wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) kutoka Makao Makuu,, Peter Lwanda. Uzinduzi ukiendelea. Wataalamu kutoka TASAF wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya ya Manyoni wakati wa uzinduzi huo. Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Manyoni ikiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya hiyo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TASAF na Viongozi wa Halmashauri. Uz

Mwakinyo kumpa asante Rais Samia kwa kumchapa Mayala

Image
  Bondia Hassan Mwakinyo ameahidi kumpa kipigo kikali mpinzani wake  Antonio Mayala kutoka Angola ikiwa asante kwa Rais wa kwanza mwanamke wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan. Mwakinyo ambaye atawania mkanda wa Afrika (ABU) wa uzito wa Super welter atapanda ulingoni  kesho kwenye ukumbi wa Next Door Arena, Masaki katika pambano lililoandaliwa na kampuni ya Jackson Group Sports. Alisema kuwa amejiandaa vyema na kwa vile atakuwa anapigana kwa mara ya kwanza chini ya uongozi wa Rais Samia, hatofanya makosa zaidi ya kushinda katika raundi  za mwanzoni tu katika pambano hilo lililodhaminiwa na KCB Bank, Plus TV, Multichoice Tanzania, Tanzania Tourism Board, Onomo Hotel, Precision Air, Prestine Logistics, Urban Soul na washirika wa kimataifa Global Boxing Stars na Epic Sports Entertainment. “Nitakuwa napigana kwa mara ya kwanza chini ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan. Sitamwangusha Rais na watanzania kwa ujumla, nawaomba mashabiki kufika kwa wingi ili kunipa sapoti,” alisema Mwakinyo. Wakati

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI MEI 27, 2021

Image
 

TANZANIA YAPATA MKOPO WA DOLA MILIONI 140 KUTOKA AfDB KUTEKELEZA MRADI WA UMEME MTO MALAGARASI, KIGOMA

Image
  Na, Saidina Msangi na Ramadhani Kissimba, WFM, Dar es Salaam Serikali ya  Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Afrika zimesaini  mikataba miwili ya mkopo wenye thamani ya dola za Marekani milioni 140 (takriban shilingi bilioni 323.4) kwa ajili ya kufadhili Mradi wa kufua Umeme wa nguvu ya maji -  Malagarasi.     M i kataba  y a  mkopo huo wenye masharti nafuu imesainiwa  Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Serikali na Bi. Nnenna Nwabufo,   Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Kanda ya Afrika Mashariki .   Akizungumza wakati wa kusainiwa kwa M i kataba hiyo, Bw. Tutuba  alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo   utaijengea TANESCO uwezo wa usambazaji wa vifaa vya kuunganisha wateja 4,250 katika Wilaya za Kigoma, Kibondo na Kasulu ikiwemo kaya 1,000 zenye kipato cha chini, zahanati 4 na shule za msingi 6.   “Mradi huu utahusisha ujenzi wa kituo kipya cha uzalishaji wa umeme wa gridi ya 49.5 MW chenye uwezo wa   kuzalis

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO MEI 26, 2021

Image