Posts

SERIKALI YASAINI MKATABA WA MRADI WA MAJI KUTOKA ZIWA VICTORIA KWENDA MIJI YA TINDE NA SHELUI

Image
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga (kushoto) na Naibu Meneja    Mkuu wa Kampuni ya Megha Engineering and Infrastructures Ltd katika Miji ya Tinde na Shelui ,bwana Murali Mohan  wakitia Saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda katika Miji ya Tinde na Shelui.

SEKTA YA HIFADHI YA JAMII KUCHOCHEA KASI YA MAENDELEO YA KIUCHUMI NCHINI

Image
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (kushoto) akizungumza na wasimamizi wa mradi wa Kiwanda cha Machinjio ya Kisasa cha Nguru Hills pamoja na Viongozi wa Mkoa na Ranchi hiyo ya Nguru Hills alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo Mvomero, Mkoani Morogoro. Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo. Na. Mwandishi Wetu – Morogoro Imeelezwa kuwa Sekta ya Hifadhi ya Jamii ikitumika vizuri itawezesha kukuza kasi maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi na taifa kwa ujumla endapo itawekeza kwenye maeneo au miradi ya kimkakati. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama wakati akitoa majumuisho ya ziara yake alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa Kiwanda cha Machinjio ya Kisasa cha Nguru Hills kilichopo Mvomero, Mkoani Morogoro. Akik

GEKUL AMSIMAMISHA KAZI MKUU WA KITUO CHA UKAGUZI WA MIFUGO RUVU DARAJANI

Image
Na Mbaraka Kambona, Pwani Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul amemsimamisha kazi Mkuu wa Kituo cha Ukaguzi wa Mifugo cha Ruvu Darajani, Gabriel Lyakurwa kwa tuhuma za kutorosha mifugo na kusababisha upotevu wa mapato ya Serikali, huku akimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi, Evarist Ndikilo kuwachukulia hatua Watumishi waliochini ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo ambao walikuwa wanashirikiana na Mkuu huyo wa kituo.   Gekul alitoa maamuzi hayo baada ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani kuibua tuhuma hizo katika ziara yake aliyoifanya kwenye kituo hicho kilichopo Ruvu Darajani, Wilayani Bagamoyo Februari 24, 2021. Mhandisi Ndikilo alisema uchunguzi alioufanya umebaini kuwa Mkuu wa kituo hicho amekuwa akishirikiana na wenzake wasiowaaminifu kutorosha mifugo inayopelekwa katika kituo hicho kwa ajili ya kukaguliwa kabla ya kuruhusiwa kupelekwa katika maeneo mengine ya minada. “Mhe. Naibu Waziri nimefanya uchunguzi wa kina na kugundua kuwa utoroshaji huu unahusisha mt

HALMASHAURI NAMTUMBO YAMCHEFUA NAIBU WAZIRI MABULA KWA KUANDAA HATI NNE KWA MIEZI NANE

Image
Na  Munir Shemweta, WANMM SONGEA Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amekerwa na halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma kuandaa Hati za Ardhi nne katika kipindi cha miezi nane tangu kuanzishwa kwa ofisi ya Ardhi mkoa wa Ruvuma. Aidha, Naibu Waziri wa Ardhi ameonesha kutoridhishwa na kasi ya utoaji hati katika halmashauri zote za mkoa wa Ruvuma ambapo katika kipindi cha miezi nane halmashauri za mkoa huo zimeandaa jumla ya hati 623. Akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi na wakurugenzi wa halmashauri za mkoa wa Ruvuma tarehe 24 Februari 2021 katika kikao kazi cha kuzungumzia masuala ya ardhi na kuhamasisha ulipaji kodi ya pango la ardhi, Dkt Mabula alisema haiingii akilini halmashauri kuandaa hati nne kwa miezi nane huku halmashauri hiyo ikiwa na watendaji wanaolipwa mishahara. Alisema, katika kuhakikisha halmashauri za mkoa wa Ruvuma zinaongeza kasi ya utoaji hati ni lazima wakurugenzi wa halmashauri hizo kuwawekea malengo watendaji wa s

NHC KUANZA KUWAFUATILIA WADAIWA SUGU

Image
  Na Munir Shemweta, WANMM SONGEA Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limewataka wapangaji wa nyumba zake wanaodaiwa kodi na kushindwa kulipa kutokana na changamoto mbalimbali kufika ofisi za shirika hilo ili kuangalia namna bora ya kufanikisha kulipa kiasi cha fedha wanazodaiwa kabla ya kuanza kuchukua hatua za kisheria ikiwemo kuwafukuza katika nyumba zake. Meneja Huduma kwa Jamii wa NHC Bw. Muungano Saguya alisema, baada ya Shirika hilo kuwataka wapangaji wake wanaodaiwa kodi za nyumba zake wawe wamekamilisha kulipa madeni kufikia januari 30 mwaka huu, wapangaji hao wanaodaiwa wameanza kuitikia wito huku wengine wakiwa bado hawajakamilisha kulipa malimbikizo wanayodaiwa.  Akizungumza mbele ya watendaji wa sekta ya ardhi na Wakurugenzi wa halmashauri za mkoa wa Ruvuma tarehe 24 februari 2021 mkoani Ruvuma wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, Bw. Saguya alisema, ni vizuri wale wadaiwa wenye changamoto za malipo wakaenda ofisi za shir

CHUO CHA ABC BIBLE COLLEGE AND TRAINING CENTER CHAFANYA MAHAFALI YAKE YA KWANZA

Image
Mgeni rasmi katika mahafali ya kwanza ya Chuo cha ABC Bible College and Training Center kilichopo jijini Dar es Salaam, Askofu Dkt.John   Mwakilema Mkuu  wa Chuo  cha Zoe Institute of Apostolic Testmony and Seminary (ZIAT),  (kulia mbele mwenye joho jekundu) akiongoza maandamano wakati wakiingia kanisani kuanza mahafali hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki. Nyuma yake ni Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing  Center (ABC)   Flaston Ndabila  na kushoto ni Askofu  Mkuu  James Mwaipyana wa Kanisa la Glory  Temple Church  International . Mgeni rasmi katika mahafali hayo, Askofu Dkt.John   Mwakilema Mkuu  wa Chuo  cha  Zoe Institute of Apostolic Testmony and Seminary (ZIAT), akimkabidhi cheti Naomi Mushi mmoa wa wahimu wa    masomo ya kuhudumia jamii hasa watu wanaokuwa katika majanga mbalimbali ikiwemo mafuriko. Kushoto ni   Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing  Center (ABC)   Flaston Ndabila. Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing  Center (ABC)   Flaston Ndabila

Benki ya CRDB yazindua huduma ya ‘Benki ni SimBanking’ jijini Mwanza

Image
  Katika kuendelea kuboresha huduma zake, benki ya CRDB Kanda ya Ziwa imezindua huduma ya Benki ni SimBanking 'Mzigo Umeboreshwa inayowawezesha wateja wake kupata huduma za kifedha popote walipo kupitia simu zao za mkononi. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Februari 25, 2021 katika tawi la Rock City Mall jijini Mwanza, Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa Lusingi Sitta alisema huduma hiyo inawarahisishia wateja kutoa pesa, kuhamisha pesa, kufanya malipo ya Serikali huku pia usalama wa akaunti ya mteja ukiimarishwa zaidi. Aidha Sitta aliongeza kuwa huduma nyingine zilizoboreshwa ni urahisi wa kupata mikopo mbalimbali, taarifa za mihamala ya fedha, kutoa pesa kwa mawakala na mashine za ATM bila kuwa na kadi ya benki na hivyo kuwahimiza wananchi kuchangamkia huduma hiyo kwani sasa hakuna sababu ya kwenda ndani ya benki kufuata huduma za kifedha kwa kuwa zote zinapatikana kiganjani. Naye Meneja Biashara Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Japhary Hassanaly alisema wateja wa benki hiyo wa