Posts

WAJUMBE WA BODI YA MKURABITA WATEMBELEA KITUO JUMUISHI CHA BIASHARA NJOMBE

Image
KAMATI ya Uongozi ya Mpango wa Urasimishaji Ardhi na Biashara za Wanyonge Tanzania (Mkurabita), ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Balozi mstaafu Daniel Ole Njoolay imetembelea Kituo Jumuishi cha Biashara kilichopo Halmashauri ya Mji wa Njombe. Walipofika katika kituo hicho walielezwa na Afisa Biashara wa Halmashauri, George Mwaseba kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa katika kituo hicho ambacho kimewezeshwa na Mkurabita samani na vitendea kazi vikiwemo kompyuta 3, scanner, Printer na meza ambavyo vimerahisisha kazi na kuifanya halmashauri kuongeza mapato kupitia malipo ya leseni za biashara. Mwaseba amesema uwepo wa kituo hicho umewapunguzia usumbufu wananchi kwani sasa huduma karibu zote zinapatikana hapo. Mwenyekiti wa Bodi ya Mpango wa Urasimishaji wa Ardhi na Biashara za Wanyonge Tanzania  (Mkurabita), Balozi mstaafu Daniel Ole Njoolay (kushoto) pamoja na wajumbe wa bodi hiyo, wakipata maelezo kutoka kwa Afisa Biashara wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, George Mwaseba  kuhusu Kitu

THUBUTU AFRICA YAANZA KUJENGA CHOO CHA KISASA SHULE YA MWAMAGUNGULI 'A' SHINYANGA

Image
  Mkurugenzi wa Shirika la Thubutu Africa Initiatives, Jonathan Manyama akisaini Mkataba wa kazi ya ujenzi wa choo cha shule ya msingi Mwamagunguli 'A' iliyopo katika kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga itakayofanywa na fundi ujenzi Robert Kayange mkazi wa kijiji cha Galamba kata ya Kolandoto.

MAJALIWA: VIONGOZI WA SEKTA YA UMMA NA BINAFSI WAENDELEZWE

Image
*Asema lengo ni kukuza ubunifu, weledi na maadili ili kuongeza tija kwa Taifa WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema viongozi wote wa Sekta za umma na binafsi wanatakiwa waendelezwe kitaaluma kwa ajili ya kukuza weledi, ubunifu na maadili ili waweze kusimamia ipasavyo maendeleo na kuongeza tija na mapato ya Taifa. Amesema katika kipindi hiki ambacho nchi imeingia katika uchumi wa kati, Serikali ingependa kuona nguvukazi katika ngazi mbalimbali inaimarishwa na kuhakikisha viongozi wanatumia ujuzi na weledi katika maeneo ya usimamizi wa rasilimali watu, rasilimali fedha na miradi. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Januari 29, 2021) katika Mahafali ya Wahitimu wa Programu ya Uanagenzi kwa Maafisa Watendaji Wakuu (Ceo Apprenticeship Program) yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro, Dar-Es-Salaam. “Dhana ya uanagenzi ni suluhisho la kuhakikisha wataalamu wetu wanajengewa ujuzi unaohitajika mara kwa mara ili kuwaongezea umahiri katika utekelezaji wa majukum

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI JANUARI 30, 2021

Image
 

RAIS MHE. DKT. MAFUFULI AZINDUA MRADI WA MAJI ISAKA-KAGONGWA MKOANI SHINYANGA

Image
 

FEDHA ZACHELEWESHA NHC KUKAMILISHA MRADI HOSPITALI YA RUFAA MARA

Image
  FEDHA ZACHELEWESHA NHC KUKAMILISHA MRADI HOSPITALI YA RUFAA MARA    Na  Munir Shemweta, WANMM MUSOMA   Imebainika kuwa kuchelewa kupelekwa fedha katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mara iliyopo eneo la Kwangwa kumesababisha Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kutokamilisha mradi huo kwa wakati.   Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mara ulianza kujengwa  na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Septemba 15, 2019 na kutarajiwa kukamilika Agosti 2020 ambapo hata hivyo Mkandarasi (NHC) aliomba kuongezewa muda wa miezi sita (6) kutokana na kazi zilizoongezeka nje ya mkataba pamoja na kuchelewa kupatikana Wakandarasi maalum wa mradi.   Akiwa katika ziara ya siku moja katika mkoa wa Mara tarehe 28 Januari 2021 kukagua utendaji wa sekta ya ardhi na kuhamasisha ukusanyaji kodi ya Pango la ardhi, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula  alielezwa na Katibu Tawala wa mkoa Mara Catherine Mthapura akiwa kwenye ofisi ya Mkuu wa mkoa kuwa, a

SERIKALI: TUNACHUKUA HATUA MADHUBUTI KULINDA NGUVUKAZI YA NCHI

Image
  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Watu wenye Ulemavu, Ummy Nderianaga, akiwahutubia washiriki wa mafunzo ya Huduma ya Kwanza ambao ni watumishi wa TANESCO alipohitimisha mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Mwanza. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Watu wenye Ulemavu, Ummy Nderianaga, akikabidhi vyeti kwa washiriki wa mafunzo ya Huduma ya Kwanza ambao ni watumishi wa TANESCO alipohitimisha mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Mwanza. Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda, akitoa maelezo ya awali mbele ya Mgeni Rasmi (Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Watu wenye Ulemavu) wakati wa kufunga mafunzo ya Huduma ya Kwanza yaliyotolewa na OSHA kwa watumishi wa TANESCO. Mkufunzi kutoka OSHA, Nathanael Mbwambo, akifundisha somo la Huduma ya Kwanza kwa vitendo katika mafunzo hayo yaliyotolewa kwa watumishi wa TANESCO jijini Mwanza. ******************************************** Na Mwandishi Wetu Serikali imes