Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Habari Lajionea Ujenzi wa SGR
Na Shamimu Nyaki -WHUSM, Morogoro. Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa metembelea M radi wa K imkakati wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro - Dodoma ambapo wamefurahishwa na namna mradi huo unavyotekelezwa kwa kasi. Akizungumza kwa niaba ya baraza hilo , Novemba 27, 2020 Mkuu wa msafara ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. Petro Lyatuu , amesema kwamba ziara hiyo imekuwa na manufaa kwa kuwa wajumbe wa baraza wamejifunza kwa vitendo namna mradi unavyotekelezwa hatua kwa hatua. "Tumekua na siku nzuri leo tumejifunza kwa kuona jinsi Serikali inavyotekeleza mradi huu, tumeona hatua il i yofikiwa katika ujenzi ikiwemo usimikwaji wa nguzo za umeme pamoja na utandikaji wa mataruma ya reli, naamini tutakua mabalozi wazuri katika kuelimisha na kushawishi wengine waje wajifunze na kuona kazi inayofanyika hapa" amesema Bw. Lyatuu. Kwa upande wake Mhandisi Msaidizi wa Mradi kutoka Shirika la Reli Tanzan