Posts

RAIS SAMIA AWASILI KIGALI NCHINI RWANDA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kigali Nchini Rwanda kwa ajili ya kuanza ziara rasmi ya Kiserikali ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais wa Nchi hiyo Mhe. Paul Kagame leo Agosti 02,2021.  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU AGOSTI 2, 2021

Image
 

MBUNGE KINGU ACHANGIA MIFUKO 20 YA SARUJI KANISA LA KKKT

Image
  Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT)  Dayosisi ya Kati, Mchungaji Dkt. Syprian Hilinti (kushoto) akizungumza katika harambee ya ujenzi wa nyumba ya Mchungaji wa Kanisa hilo Usharika wa Chungu lililopo Ihanja wilayani Ikungi mkoani Singida. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu Wachungaji wa kanisa hilo wakiwa kwenye harambee hiyo. Waumini  wakiwa kwenye harambee hiyo. Na Dotto Mwaibale, Ikungi MBUNGE wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu amechangia saruji mifuko 20 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Usharika wa Chungu lililopo  Ihanja wilayani Ikungi mkoani Singida. Kingu ametoa msaada huo wakati wa harambee iliyofanyika katika kanisa hilo leo hii ambayo iliongozwa na Msaidizi wa Askofu wa Kanisa hilo  Dayosisi ya Kati, Mchungaji Dkt. Syprian Hilinti. Aidha katika harambe hiyo Kingu alichangia kutengeneza madirisha yote ya nyumba ya mchungaji wa ushirika huo

WACHIMBAJI WADOGO KUPOKEA KIFUTA JASHO CHA MILIONI 90 -SINGIDA

Image
Na Steven Nyamiti – Mkalama Singida Jumla ya Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu 90 katika eneo la kijiji cha Tumuli wataanza kupokea kifuta jasho kuanzia  tarehe 2 Agosti, 2021 baada ya utaratibu wa kupewa kifuta jasho kukamilika. Hayo yameelezwa na Waziri wa Madini Doto Biteko tarehe 31 Julai, 2021 katika kijiji cha Tumuli wilaya ya Mkalama Mkoani Singida wakati wa ziara ya kukagua na kutembelea shughuli za wachimbaji wadogo. Ameeleza kuwa, wachimbaji watakaopokea kifuta jasho hicho ni wale walioandikishwa na ambao taarifa zao zipo kwenye Kanzidata kufuatia kuondolewa kuchimba kwenye eneo lenye leseni. “Mgogoro huu una historia ndefu sana zaidi ya miaka 9, mwanzo walikua wachimbaji 26 wanaopaswa kupewa  lakini sasa wameongezeka zaidi ya 100, lazima tutende haki kwa watu wote kuanzia mchimbaji  hadi mwekezaji ili pande zote ziridhike,” amesema Biteko. Aidha, Waziri Biteko ameagiza mgodi wa Chama cha Ushirika cha Uchimbaji Madini (Sekenke One Mining Cooperative Society) uliosimamish

SUA, NEMC WAJIPANGA KUTAFUTA SULUHISHO LA UHARIBIFU WA VYANZO VYA MAJI NA MAZINGIRA BONDE LA MTO RUFIJI

Image
  Mkurugenzi wa Masomo ya Shahada za juu utafiti uhauwilishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitaalamu SUA,     Prof. Esron Karimuribo akitoa salamu za Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wakati wa uzinduzi wa mradi wa  “usimamizi endelevu wa madakio ya maji kupitia tathmini ya kuimarisha mtiririko wa maji kwa mazingira na utekelezaji wake katika kulinda Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi iliyofanyika wilayani humo mkoani Mbeya juzi. Meneja Tafiti za Mazingira kutoka NEMC ambaye pia ni Mtafiti Mkuu mwenza wa mradi huo, Rose Mtui akitoa neno la ukaribisho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu (NEMC) Mhandisi Dkt. Samuel Mafwenga. Mratibu wa mradi Dkt. Winfred Mbungu akitambulisha mradi huo wa EFLOWS kwa wadau ili kujua utekelezaji wake,malengo yake na matarajio yake utakapokamilika. Mtafiti  M kuu wa mradi huo wa EFLOWS Prof. Japhet Kashaigili ambeye pia ni Mratibu wa tafiti na machapisho SUA akieleza malengo la Warsha hiyo ya siku moja ya wadau. Mkuu wa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, Reub

RC KUNENGE AWAASA WAHITMU KADA YA AFYA KUZINGATIA MAAFILI

Image
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe Abubakar Kunenge amewataka wahitimu kada ya afya kuhakikisha wanasimamia maadili ya kazi yao kutokana na kazi yao kushughulikia zaidi na maisha ya watu. Mhe.Kunenge ameyasema hayo leo Julai, 30 2021 alipohudhuria mahafali ya 54 ya chuo cha Tiba na Sayansi Shirikishi kilichopo Kibaha. "Katika taaluma ambazo mtumishi anatakiwa kuwa na nidhamu ni hii ya afya kwasababu mnashughulika zaidi na afya  maisha ya watu hakika hapa mnatakiwa kuwa na maadili" alisema. Alisema anahitaji kuona wahitimu hao wakisifiwa kwa kuwa na nidhamu katika maeneo watakayoenda kufanya kazi na kwamba hiyo itakuwa heshima kwake  Katika mahafaali hayo wahitimu 94 walikabidhiwa vyeti vya kuhitimu na Mh. Kunenge.  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI AGOSTI 1, 2021

Image