Posts

JESHI LA POLISI LIMETOA MAFUNZO KWA MAFUNDI WA MAGARI

Image
  Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi kitengo cha Usalama barabarani, limetoa mafunzo kwa mafundi magari waliyokuwa ndani ya Kituo cha Mabasi cha Magufuli, Mbezi Luis, Dar es Salaam kwa lengo la kuwafundisha jinsi ya kutambua vifaa ambavyo vipo kwenye magari hayo. Mafunzo hayo yametolewa leo Mei 29, 2021 na Mkuu wa Usalama Barabarani, ASP Ibrahim Samwix ,kwa lengo la msfundi hao kutambua mfumo wa injini ya gari unavyofanya kazi ili kuwaraisishia namna ya utengenezaji wa magari. Pia,Mkuu huyo  aliwafundisha kuhusu kifaa cha aina ya turbo kinavyofanya kazi, na namna ya kukitambua kama kikiwa  kibovu, kwa sababu mafundi wengi wamekuwa wakifanya masuala ya ufundi kwa mazoea. ASP Samwix alitoa pia mafunzo katika kifaa cha mfumo wa rejeta namna kinavyofanya kazi, kwa sababu mafundi wengi na madereva wamekuwa wakishindwa kutunza mabasi wanayopewa kutokana na mapungu madogo madogo. Kabla ya mafunzo hayo, Mkuu huyo alianza na madereva kwa kuelimisha jinsi ya kufuata sheria za barabarani na kuende

MKUU WA MAJESHI JENERALI VENANCE MABEYO ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA- PRETORIA

Image
 Leo Jumamosi tarehe 29 Mei, 2021. Mkuu wa Majeshi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo, alitembelea Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika Kusini. Jenerali Mabeyo yupo Nchini Afrika Kusini kuhudhuria sherehe za kumuaga Mkuu Majeshi wa Afrika Kusini Jenerali Solly Zacharia Shoke zilizofanyika kitaifa Jana Mjini Pretoria. Kuhudhuria sherehe hizi, ni utaratibu uliowekwa na nchi wanachama wa Jumuiya za SADC ya maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika kuimarisha mashirikiano hususan katika Nyanja ya Diplomasia ya Ulinzi (Defence Diplomacy) na Amani katika eneo la nchi za SADC. Jenerali Mabeyo, alikaribishwa Ubalozini na Mhe. Balozi Mej. Jen. Gaudence Salim Milanzi (Mst) na watumishi wa Ubalozi, Mhe. Balozi Milanzi alitoa taarifa fupi ya eneo la uwakilishi ya Afrika Kusini, Botswana na Falme ya Lesotho. Katika taarifa hiyo, Mhe. Balozi alieeza kuwa hali ya uwakilishi inaridhisha kiulinzi na kiusalama, Ubalozi umeendelea kukuza mashirikiano na nchi za e

CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE (TAWLA) CHAFANYA MKUTANO MKUU WA 31 WA MWAKA

Image
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson Mwansasu akizungumza katika mkutano wa 31 wa mwaka wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) unaofanyika kwenye Hoteli ya Coral Beach Masaki mkoani Dar es Salaam leo Jumamosi 29,2020. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson Mwansasu akizungumza katika mkutano wa 31 wa mwaka wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) unaofanyika kwenye Hoteli ya Coral Beach Masaki jijini Dar es Salaam leo Jumamosi 29,2020 Katikati ni  Lulu Ngw'anakilala Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWLA na kushoto ni Mwanachama wa TAWLA Flaviana Charles Rwechungura. Balozi Mwanaidi Maajal Mwanachama wa (TAWLA) akiongoza mjadala katika mkutano huo unaofanyika kwenye hoteli ya Coral Beach Masaki jijini Dar es salaam Lulu Ngw'anakilala Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (TAWLA) akimkaribisha mgeni rasmi ili kuzungumza na wanachama wa taasisi hiyo katika mkutano huo. Naibu

RC KUNENGE AWATAKA VIONGOZI WA HALMASHAURI CHALINZE KUANGALIA VYANZO VINGINE VYA MAPATO

Image
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amewataka watumishi wa Halmashauri ya Chalinze kuangalia namna ya kubuni vyanzo vingine vya mapato ili kuongeza makusanyo ya Halmashauri hiyo. Kunenge ametoa rai hiyo alipokuwa akiongea na watumishi wa Halmashauri hiyo katika ziara yake ya kujitambulisha kwenye Wilaya ya Bagamoyo mkoani humo. " Siendi kwenye mapato ya jumla naangalia vyanzo maelekezo yangu muangalie namna ya kuongeza vyanzo vingine ili kuongeza makusanyo" alisema Kunenge. Kunenge pia aliongea na Madiwani wa Halmashauri hiyo kusikiliza kero zilizopo kwenye kata zao ili atafute namna ya kuzifanyia kazi baada ya kukamililisha ziara yake kwenye Wilaya na Halmashauri za Mkoa huo. Aliahidi kujenga ushirikiano na wabunge, Madiwani na watumishi ili kufikia lengo la kuwaondolea wananchi kero zinazowakabili. Katika  ziara hiyo Kunenge alipokea madawati 390 kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambayo yamelenga kupunguza uhaba wa madawati kwenye shule za Hal

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI MEI 29, 2021

Image
 

RC KUNENGE ATOA ONYO KWA WATENDAJI WA BODI YA MAGHALA NA WAKALA WA VIPIMO

Image
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge ametoa Onyo  kwa watendaji wa Bodi ya Maghala na Wakala wa Vipimo kwa kushindwa kupima mizani zilizopo kwenye  maghala ya Msingi  zinazotumika kupokelea Ufuta na  kushindwa kusimamia maandalizi ya Maghala Makuu, hali inayopelekea kero na kusuasua kwa zao hilo. Ameyasema hayo leo Mei, 26 2021 wakati akiendesha Mkutano wa Wadau wa Ufuta Mkoani hapo, Mkutano huo umefanyika Ikwiriri Wilayani Rufiji. "Natoa Onyo kwa  watendaji wa Serikali siihitaji Ubabaishaji' Changamoto katika zao la  ufuta chanzo pia ni ninyi  Watumishi wa Serikali. Amesema hafurahishwi  na Watendaji hao wa Serikali kusubiri kuitwa na  Wakulima badala ya kuwafuata na kutoa huduma. Ameeleza hatosita kuwaondoa Mkoani hapo kwa kushindwa kusimamia wajibu wao kikamilifu. Aidha, RC Kunenge ametoa siku tatu kwa watendaji hao  kwamba hadi kufikia Mei 28, 2021 kuhakisha kuwa wanakamilisha maandalizi ya Maghala  Makuu na Upimaji wa Mizani kwenye maghala ya Msingi.  

WAZIRI MHAGAMA: TATIZO LA AJIRA NCHINI KUFANYIWA UTAFITI

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, akisisitiza umuhimu tafiti za nguvu kazi na Rasilimali watu,  wakati akifungua Kongamano la Wadau wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo  leo tarehe 27 Mei, 2021, Jijini Dodoma.   Katika kuhakikisha malengo ya kutatua masuala ya ajira na kazi, yanafikiwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), imepanga mwaka huu kufanya tafiti mbili kubwa ambazo zitajikita kwenye kubaini nguvu kazi pamoja na rasilimali watu. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, wakati akifungua Kongamano la Wadau wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo  leo tarehe 27 Mei, 2021, Jijini Dodoma. Ameeleza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi