Posts

MAKAMU WA RAIS MTEULE AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

Image
  Na Josephine Majura na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma. Makamu wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, amekutana na Watumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango na kuwasisitiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii kutokana na umuhimu wa Wizara hiyo katika maendeleo ya nchi. Mheshimiwa Philip Isdor Mpango, ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango, alitoa rai hiyo jijini Dodoma alipokutana na watumishi wa Wizara hiyo katika ofisi zilizopo Treasury Square, akitokea bungeni baada ya kuteuliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Bunge kuthibitisha uteuzi wake kwa kura za kishindo. Dkt. Mpango amewataka watumishi wa wizara hiyo kuendelea kufanya kazi kwa weledi kwa kuwa wizara hiyo ni moyo wa Serikali na kwamba wasipofanya kazi vizuri na kwa uaminifu hakuna miradi ya maendeleo itakayotekelezwa, mishahara haitapatikana wala mikopo itakayokopwa hivyo kukwamisha maendeleo ya wananchi. Alisema hana shaka na uwezo wa viongozi na wataalam

TMA YAWATOA UKUNGU WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UTABIRI WA HALI YA HEWA NA TAFITI

Image
Ladslaus Chang"a Mkurugenzi wa Huduma za Utafiti na Matumizi Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) akifungua semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu taarifa mbalimbali za utabiri wa Hali ya hewa tafiti na matumizi ya taarifa hizo inayofanyika kwenye ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) Kibaha Mkoani Pwani. Monica Mutoni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali katika semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu taarifa mbalimbali za utabiri wa Hali ya hewa tafiti na matumizi ya taarifa hizo inayofanyika kwenye ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) Kibaha Mkoani Pwani. Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada katika semina hiyo kuhusu taarifa mbalimbali za utabiri wa Hali ya hewa tafiti na matumizi ya taarifa hizo inayofanyika kwenye ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) Kibaha Mkoani Pwani. Kulia ni Joyce Makwata Mchambuzi

KAMATI KUU YA CCM YAKETI DODOMA

Image
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo March 30,2021 ameshiriki katika kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambacho ni kikao Maalum kinachoendelea Makao Makuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Jijini Dodoma.  

USAJILI WA VIKUNDI VYA KIJAMII VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA KIELEKTRONIKI

Image
 

RAIS SAMIA AMTEUA DKT. PHILIP ISIDOR MPANGO KUWA MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA

Image
 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Philip Mpango (pichani) kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, SPIKA wa Bunge Mhe. Job Ndugai ameliambia Bunge jijini Dodoma leo Machi 30, 2021. Dkt. Mpango alikuwa WAZIRI wa Fedha na Mipango na Mbunge wa Jimbo la Buhigwe mkoani Kigoma. Bunge linatarajiwa kumpitisha KATIKA kikao kinachoendelea kwa kumpigia kura ambapo inatakiwa wabunge ASILIMIA 50 wamuunge mkono. Wabunge 363 wamepiga kura na hakuna kura iliyoharibika na hakuna kura ya hapana hata moja. Kwahiyo amepata ASILIMIA 100 ya kura zote.

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE MACHI 30, 2021

Image
 

SIMBACHAWENE AWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI KWA KIPINDI CHA MWAKA 2020/2021 NA MPANGO WA BAJETI 2021/2022 JIJINI DODOMA.

Image
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akiwasilisha  Taarifa za Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Kipindi cha Mwaka 2020/21 na Mpango wa Bajeti 2021/22 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama jijini Dodoma leo . Inspekta Jenerali wa Polisi,Simon Sirro  akizungumza wakati wa Uwasilishaji wa   Taarifa za Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Kipindi cha Mwaka 2020/21 na Mpango wa Bajeti 2021/22 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama jijini Dodoma leo Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza,Suleiman Mzee,   akizungumza wakati wa Uwasilishaji wa   Taarifa za Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Kipindi cha Mwaka 2020/21 na Mpango wa Bajeti 2021/22 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama jijini Dodoma leo Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dkt.Anna Makakala   akizungumza wakati wa Uwasilishaji wa   Taarifa za Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Kipindi cha Mwaka 2020/21 na Mpango wa Bajeti 2021/2