Posts

SERIKALI IMETENGA MEGAWATI 70 ZA UMEME KUENDESHA TRENI YA MWENDOKASI, DKT. KALEMANI ASEMA HATA LEO TRENI IKIWA TAYARI UMEME UPO.

Image
NA K-VIS BLOG, MOROGORO WAZIRI wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani amesema Serikali kupitia TANESCO tayari imetenga Megawati 70 za umeme wa kuendesha treni ya mwendokasi maarufu SGR. Mhe. Dkt. Kalemani ameyasema hayo leo Februari 27, 2021 wakati akifungua rasmi kikao kazi cha TANESCO na Wahariri wa vyombo vya habari kwenye ukumbi wa NSSF mkoani Morogoro. Mahitaji halisi ya kuendesha treni hiyo ya umeme ni Megawati 27. “Tunampongeza sana Rais wetu kwa kuamua kujenga SGR, hata treni hiyo ingekuwa tayari leo treni hiyo ingeendeshwa kwa umeme bila mashaka yoyote.” A.lisisitiza. Alisema tayari miundombinu ya umeme kiasi cha kilomita 160 ikiwa ni pamoja na kuweka nguzo na nyaya za umeme kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro imekamilika na kwamba kinachosubiriwa ni kuiunganisha treni hiyo na umeme wa TANESCO. Akizungumzia hali ya umeme nchini kwa sasa, Mhe. Waziri amewahakikishia watanzania na wawekezaji wa ndani na nje kuwa umeme wa kuhakikisha unaendesha uwekezaji wao upo wa kutosha na wa uha

WAZIRI MHAGAMA ATEMBELEA KIWANDA CHA MOROGORO CANVAS LTD

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiangalia moja wapo ya shuka ambazo zilikuwa zikizalishwa katika kiwanda hicho cha Morogoro Canvas Ltd. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alipowasili katika kiwanda cha Morogoro Canvas kinachomilikiwa na benki hiyo. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiwa ameambatana na Viongozi wa Mkoa wa Morogoro pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela mara baada ya kuwasili katika kiwanda hicho cha Morogoro Canvas kilichopo Mkoani Morogoro. Kulia ni Mtaalamu elekezi wa Kiwanda hicho Ndg. Dismas Machopa akitoa maelezo. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughuli

RAIS DKT. MWINYI AJUMUIKA NA WAUMINI WA KIISLAM KATIKA SALA YA IJUMAA ILIOFANYIKA MASJID RAUDHA DARAJA BOVU

Image
  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wananchi alipowasili katika viwanja vya Masjid Raudha Daraja bovu Wilaya ya Magharibi “A” Unguja kuhudhuria Ibada ya Sala ya Ijumaa iliofanyika katika msikiti huo leo 26-2-2021. IMAMU wa Masjid Raudha Daraja Bovu Wilaya ya Magharibi “A” Unguja Sheikh. Ali Faki Abdalla akizungumza na kutowa neno la shukrani kwa niaba ya Wananchi na Waumini wa Kiislam kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kufanikisha kuwamalizia ujenzi wa Masjid yao, shukrani hiyo imetolewa baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika leo.26-2-2021 katika msikiti huo.   RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, akizungumza na Waumini wa Kiislam wa Masjid Raudha Daraja Bovu Wilaya ya Magharibi “A” Unguja, baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa, iliofanyika katika Masjid hiyo leo 26-2-2021, na kupokea shukrani zao. RAIS w

WAKANDARASI WAZEMBE KUPOKONYWA MIRADI YA MAJI

Image
  Na Mohamed Saif Serikali itawapokonya na haitowapa tena kazi ya kujenga miradi ya maji Wakandarasi wanaoshindwa kuikamilisha kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa. Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi ametoa tamko hilo Februari 25, 2021 wakati wa ziara yake kwenye mradi wa maji wa wa vijiji vya Buyagu, Kalangalala na Bitoto Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza. Awali akiwasilisha taarifa ya mradi, Meneja wa Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Sengerema, Mhandisi Cassian Wittike alisema ulikuwa ukitekelezwa na Mkandarasi mzawa Kampuni ya D4N Construction Limited ya Wilayani Kahama ambaye alishindwa kuukamilisha kwa mujibu wa mkataba wake. “Mradi huu ni miongoni mwa miradi tuliyorithi kutoka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa mwaka 2019 na haukua umekamilika kutokana na uwezo mdogo wa mkandarasi,” alimueleza Naibu Waziri. Mhandisi Wittike alisema kwamba mradi ulianza kutekelezwa tangu Desemba 2013 na ulipaswa kukamilika Juni, 2014 kwa gharama ya shilingi bilioni 1.7 lakini m

TANESCO YAJA NA MFUMO "MTEJA UKINUNUA UMEME HULAZIMIKI KUINGIZA TOKEN KWENYE MITA, UNAINGIA WENYEWE MOJA KWA MOJA BAADA YA MALIPO"

Image
  SHIRIKA la Umeme nchini TANESCO linatarajia kuweka mfumo utakaomuwezesha mteja aliyenunua umeme kupitia simu ya kiganjani kutolazimika kuingiza namba (TOKEN) kwenye mita na badala yake umeme utaingia moja kwa moja kwenye mita   mara tu baada ya kukamilisha malipo. Meneja Mwandamizi Usambazaji Umeme Mhandisi Athanasius   Nangali(pichani juu) amewaambia Wahariri wa vyombo vya habari wanaoshiriki kikao kazi baina ya TANESCO na Wahariri mjini Morogoro Februari 26, 2021. “TANESCO tunaendelea kuboresha zaidi utoaji wa huduma zetu na sasa hivi tuko kwenye mpango wa kuweka mfumo ambapo mteja atakaponunua umeme kwenye simu yake au kwingineko basi umeme utaingia moja kwa moja kwenye mita yake nyumbani na hatalazimika tena kuingiza namba (TOKEN) kwenye mita.” Mhandisi Nangali amefafanua. Akifafanua zaidi alisema TANESCO tayari imemuajiri mtaalamu mshauri kutoka serikalini ili akague specification na akishamaliza kuzikagua tunaingia kwenye huo mfumo moja kwa moja. “Lengo letu sisi tunata

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI FEBRUARI 27, 2021

Image