Posts

KATIBU TAWALA MKOA WA SINGIDA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA SEKTA YA ELIMU

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Singida  Dk. Angelina Lutambi, akizungumza na wakuu wa shule za sekondari na maafisa elimu kata katika kikao kazi kilichofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Mwenge mkoani hapa. Afisa Elimu Mkoa wa Singida, Nelasi Mulungu,   akizungumza kwenye kikao hicho. Kikao kikiendelea.   Na Mwandishi Wetu, Singida KATIBU Tawala Mkoa wa Singida  Dk. Angelina Lutambi amewataka wakuu wa shule na maafisa elimu kata mkoani hapa kufanya kazi kwa bidii ili kubadilisha mitazamo ya jamii zinazozunguka shule zao.  Lutambi aliyasema hayo jana katika kikao kazi cha wakuu wa shule zote za Sekondari na maafisa elimu kata kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Mwenge ambacho kililenga kufanya tathimini ya matokeo ya kidato cha nne na kidato cha pili Mwaka 2020. Katibu Tawala huyo alisema wakuu wa shule ni  chachu ya mabadiliko kwenye jamii inayowazunguka ,wanafunzi wanapomaliza shule na kurudi kwa jamiii hivyo kama jamii haijabadilika ni isha

MIGODI YA BUZWAGI NA BULYANHULU YALIPA USHURU SH. BIL 2.3 MANISPAA YA KAHAMA NA MSALALA DC

Image
  Meneja Mkuu wa Migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi, Benedict Busunzu (wa tatu kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha ( wa pili kushoto) hundi ya shilingi 744,929,725.78  kwa ajili ya Halmashauri ya Msalala ambazo ni malipo ya ushuru kwa ajili ya maendeleo leo Jumamosi Januari 30,2021. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala, Simon Berege. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

DKT.KIJAZI AWATAKA WATUMISHI KUFANYA MAZOEZI

Image
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi akimvisha medali Afisa Rasilimaliwatu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Stella Msuya ikiwa ni moja ya pongezi ya kushiriki bonanza la watumishi lililoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lililofanyika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo. Washiriki wa mchezo wa mbio za magunia wakichuana wakati wa bonanza la watumishi lililoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lililofanyika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo. Na Happiness Shayo –Dodoma Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi amewataka watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao na kujenga mshikamano na upendo katika maeneo yao ya kazi. Dkt. Kijazi ametoa wito huo wakati wa bonanza la watumishi lililoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lililofanyika leo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mazoezi iwe ni sehemu ya maisha yetu na pia iwe ni sehemu ya kazi

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI JANUARI 31, 2021

Image
 

JPM AZINDUA MIRADI YA KIHISTORIA TABORA, NI WA MAJI NA UJENZI WA JENGO LA IMEJENSI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima, Mawaziri pamoja na viongozi wengine wakati akiweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Huduma ya Dharura katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora leo tarehe 30 Januari 2021.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga wakati akikagua ujenzi wa Matanki makubwa ya kuhifadhia maji katika mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria katika miji ya Tabora, Igunga na Nzega Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa mkoa wa Tabora katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora leo tarehe 30 Januari 2021 mara baada ya kuzindua mradi wa maji ya kutoka ziwa Victoria pamoja na jengo la huduma kwa wagonjwa wa dharura.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiw

NAIBU WAZIRI MARY FRANCIS AONGOZA MAZOEZI WILAYANI MAGU

Image
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Francis Masanja ( wa pili kutoka kushoto mbele) akiongoza mazoezi ya kutembea na kukimbia yaliyowahusisha wananchi na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu akiwemo Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Salum Kalli (,) leo tarehe 30/1/2021. Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Francis Masanja akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Magu mara baada ya  kuongoza mazoezi ya kutembea na kukimbia yaliyowahusisha pia viongozi wa Halmashauri hiyo. Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mhe. Salum Kalli akiongea na Wananchi mara baada ya kuhitimisha  mazoezi ya kutembea na kukimbia yaliyowahusisha wananchi na viongozi na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu leo Januari 30, 2021.  

NAIBU WAZIRI KUNDO ATOA WITO KWA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Image
Na Faraja Mpina - WMTH Wito umetolewa kwa wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa kuzingatia vigezo walivyojiwekea. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo  Mhandisi Andrea Kundo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo jijini Dodoma,ambapo amesema ili kutekeleza malengo ya wizara hiyo , ushirikiano wa hali ya juu unahitajika miongoni mwa viongozi wa wizara, watumishi  na wadau wa sekta ya mawasiliano kwa ujumla. Aidha,Menejimenti ya wizara hiyo imetakiwa kuhakikisha kunakuwa na mazingira mazuri na wezeshi ya utendaji kazi,mahusiano bora kazini pamoja na wafanyakazi kupata stahiki zao kwa muda muafaka na pale inaposhindikana taarifa sahihi zitolewe  kwa wakati husika. Aliongeza kuwa,  kila mtumishi anatakiwa kusoma na kuelewa sera, sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali ya utumishi wa umma na kutekeleza wajibu wao ipasavyo. “Kazi ya baraza la