Na Faraja Mpina, WUUM, Dodoma Msajili wa Hazina Athumani Selemani Mbutuka ameliagiza Shirika la Posta Tanzania (TPC) kubadilika katika utendaji wao kulingana na ushindani uliopo na mashirika mengine, kwa kuwa wabunifu kibiashara na kuweka malengo ya kuongeza ukusanyaji wa mapato hasa katika biashara yake ya duka la kubadilisha fedha (Bureau de change) ili kuhakikisha wanaongeza uzalishaji, na uchumi wa Shirika hilo unaimarika ili kuweze kutoa gawio kubwa kwa Serikali. Mbutuka aliyasema hayo alipokuwa akifunga mafunzo ya siku tano ya viongozi wakuu wa Shirika hilo yaliyofanyika katika ukumbi wa TBA jijini Dodoma. “Ili uingine katika ushindani ni lazima uwe na uwezo wa kushindana kwa kuzingatia fursa zilizopo, mahitaji ya wateja na ukuaji wa teknolojia, hasa kipindi hiki cha matumizi ya TEHAMA katika kutoa huduma mbalimbali kwa jamii. Shirika hili limepewa dhamana ya kutoa huduma nyeti na muhimu kwa Serikali na jamii, hivyo linatakiwa kuwa Shirika la mfano na lijiendeshe kwa faida kwa