9/21/2021

RC KUNENGE AANZA ZIARA YA KUTEMBELEA WILAYA ZA MKOA WA PWANI KUKAGUA MIRADI, KUSIKILIZA KERO NA KUZIPATIA UFUMBUZI

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amesema lengo la mkoa wake ni kuwa na mabaraza ya ardhi kwenye wilaya zote za mkoa huo.

Mhe. Kunenge ameyasema hay oleo Septemba 21, 2021 mwanzoni mwa ziara yake ya kutembelea wilaya zote za mkloa huo ili kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Kituo cha kwanza cha ziara yake kilikuwa ni Wilayani ya Bagamoyo Kata ya Magomeni ambapo moja ya kero kubw aliyokutana nayo kutoka kwa wananchi ni kutokuwa na baraza la Ardhi la Wilaya.

Akijibu kero hiyo RC Kunenge alisema “Mpango wa Mkoa ni kuwa na  Mabaraza ya Ardhi katika Wilaya zote kwenye mkoa wetu,  na kwakweli tumeshaunda Mabaraza hayo kwenye  Wilaya za Kibaha na Mafia,” alisema na kuongeza  …………….Wajumbe wa baraza katika Wilaya ya Mkuranga wataapishwa Jumatano hii, Wilaya ya Kisarawe Wajumbe wataapishwa Jumatatu wiki  ijayo.” Alibainisha.

RC Kunenge alisema kwa upande wa Wilaya za  Rufiji na Bagamoyo tayari Mkoa umewasilisha majina ya Wajumbe waliopendekezwa kwa Mhe. Waziri wa Ardhi na wanasubiri kurejeshewa ili waaendelee na teuzi.

Mhe Kunenge ameeleza kuwa ziara yake itapita kata kwa kata katika Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kukagua Miradi na Kusikiliza Kero za Wananchi.

Aidha Mhe. Kunenge amewahimiza Wananchi kuheshimu sheria ili kumaliza migogoro ya Ardhi Mkoani hapo.

RC Kunenge pia amepongeza kukamilika kwa  mradi wa Ujenzi wa shule ya Mchepuo wa kingereza, Kigongoni  uliogharimu Shilingi Milioni 70, ambapo kati ya fedha hizo Tsh Mil 20 zimetokana na nguvu za wananchi na Tsh Mil 50 Fedha kutoka Serikali Kuu, amewata waalimu kusimamia taaluma ya Wanafunzi hao ili wafanye vizuri bora kwenye masomo yao.

"Mkurugenzi shule hii usiiache andaeni mpango mzima master plan wa shule"

Mkoa wa Pwani  umeendelea kuanzisha Shule za Mchepuo wa Kingereza ambapo mpaka Sasa shule mbili za Serikali za Mchepuo wa kingereza Kigongoni English medium pre and Primary School  Iliyopo Bagamoyo na Mkoani Pre Primary School Iliyopo Kibaha Mjini zimeanzishwa.










 


    

0 comments:

Post a Comment