SHEHENA YA CHANJO DHIDI YA CORONA YAWASILI NCHINI

CHANJO dozi Milioni Moja ya Covid-19, imewasili nchini leo Jumamosi Julai 24, 2021.

Shehena ya Chanjo hiyo aina ya Johnson & Johnson imetolewa na serikali ya Marekani kama msaada chini ya Mpango wa COVAX, ubalozi wa Marekani nchini umesema.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, shehena hiyo imekabidhiwa kwa Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Waziri wa Afya, Dkt  Dorothy Gwajima na Balozi wa Marekani nchini, Dkt.Donald Wright.






Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"