7/01/2021

WATU 486 WAFA NCHINI CANADA KUTOKANA NA JOTO KALI

 

TORONTO, CANADA

MAAFISA nchini Canada wamesema joto kali linaloikabili nchi hiyo kwa siku tatu mfululizo limesababisha vifo vya zaidi ya watu 486.

Waziri Mkuu wan chi hiyo Justin Trudeau ametuma salamu za rambirambi kufuatia vifo hiyo.

Katika mji wa Britisha Columbia watu kadhaa wameripotiwa kufa na shughuli za dharura zimedhoofu kutokana na ongezeko la watu waliokumbwa na janga hilo kali lililokumba maeneo ya Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo na Marekani.

 

Tayari maeneo ya ndani ya jimbo hilo watu wametaarifiwa kuondoka kufikia leo Jumsatano Julai 1, 2021 .

 

Mamia ya watu wamefurika kwenye vituo 25 vya kupoza hewa jijini Vancouver ambapo watu wameketi wakisoma vitabu na wengine wakiwa kwenye laptopa wakifanya shughuli zao.

 

"Tumewahi kuwa na joto lakini sio la kiwango hiki cha sasa," alisema Lou, ambaye alijitambulisha kwa jina moja tu. "Nimeshtushwa kutokana na idadi kubwa ya vifo vilivyotokea."

“Sina kipoza hewa, ni feni tu, nimekuja hapa ili kupata ubaridi wakati nafanya kazi zangu.” Alisema. Maeneo ya Magharibi mwa Canada ndiyo yameathirika sana ambapo joto limefikia Nyuzi Joto 49.6. Mamlaka ya Hali ya hewa nchini humo imeonya kuwa joto zaidi linakuja na kuwaasa wananchi kuchukua tahadhari.

 


 


    

0 comments:

Post a Comment