5/30/2021

TANESCO YASIFIWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MIRADI.*

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limepongezwa na kusifiwa kwa utekelezaji thabiti wa Miradi mbalimbali ya Umeme ikiwemo miradi mikubwa ya kimkakati na miradi midogo midogo ya usambazaji Umeme Nchini kote. 
Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka Tarehe 30 Mei 2021 alipotembelea banda la TANESCO katika maonyesho ya Teknolojia yanayoendelea katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. 
Sambamba na pongezi hizo, Mhe Mtaka ameshauri wataalamu wa Tehama wa Shirika kushirikiana na vyuo vya elimu ya juu ili kuboresha mifumo ya utoaji huduma ikiwemo  huduma za ununuzi wa umeme wa LUKU  na kuwezesha wateja kununua umeme kisha umeme huo kuingie  katika mita  bila kumlazimu mteja kwenda kuweka umeme katika mita.
Mhe. Mtaka amesema pamoja na mambo mengi mazuri ambayo TANESCO imekuwa ikiyafanya, ni vvyema Shirika likafanya  ushirika na taasisi za elimu ya juu ili kukuza ubunifu na kuwezesha wataalamu wa ndani kutumika katika kutekeleza miradi mbali mbali bila kuhitaji wataalamu kutoka nje ya nchi na ikiwezekana wataalamu wa Shirika waweze kufanya na kusimamia hata miradi mingine mikubwa inayotekelezwa katika nchi jirani.
 “Hii nikutokana na uzowefu ambao wataalam wa TANESCO watakuwa wameupata baada ya kukamilisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati” Alisema Mhe. Mtaka

Mhe. Mtaka aliongeza kuwa, Miradi  ya umeme vijijini inatekelezwa  kwa weledi wa hali ya juu, ni vyema sasa TANESCO ikawezesha wataalam wake kwa kushirikiana na Taasisi zingine za serikali kuanza kupeleka wataamamu katika kandarasi za usimamizi wa miradi nje ya Nchi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony  Mtaka akipokea maelezo  kutoka kwa Meneja wa TANESCO  Mkoa wa Dodoma   Mhandisi Kenneth Boimanda  wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipotembelea Banda la TANESCO katika maonyesho ya teknolojia yanayo endelea katika Uwanja wa jamuhuri jijini Dodoma Leo  30 Mei 2021

Mhandisi Erasto Chiswanu akielekeza wanafunzi wa Shule Sekondari ya  Wasichana ya  Msalato jinsi Mradi wa Julius Nyerere unavyo tekelezwa  wakati wanafunzi hao walipo tembelea banda la TANESCO  katika maonyesho ya Teknolojia  yanayo endelea katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma Leo 30 Mei 2021
 

    

0 comments:

Post a Comment