PROFESA NDULU ALIKUWA MCHUMI BORA KABISA NCHINI: KIKWETE

RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete amesema mpaka sasa hakuna mchumi bora Tanzania kama Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu.

Kikwete aliyasema hayo jana nyumbani kwa marehemu Mbweni Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam alipokwenda kusaini kitabu cha maombolezo kutokana na kifo cha gwiji huyo wa uchumi kilichotokea juzi. 

Alitaja sababu ya Profesa Benno Ndulu kuwa mchumi bora kuwa ni kutokana na ujuzi na mchango wake mkubwa katika uchumi wa dunia na kutambulika kwake kulikosababisha kutumika kujenga chumi za nchi mbalimbali duniani. 

Alisema ubora wa Profesa Ndulu katika masuala ya uchumi alianza kuuona tangu akiwa Waziri wa Fedha, na kwamba, baada ya kuanzisha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mwaka 1996, alimteua Profesa Ndulu kuwa Mwenyekiti wa Bodi.

“Nilipokuwa Rais nilitamani sana Profesa Ndulu awe mshauri wangu katika masuala ya uchumi, lakini nilishindwa kumtoa katika mambo ya kimataifa ambako alikuwa tegemeo kubwa kwa Benki ya Dunia,” alisema Kikwete ambaye kitaaluma ni mchumi.

Alisema wakati huo aliamua kumuomba Profesa Ndulu ushauri kuwa ni nani anaweza kuwa mshauri wake katika masuala ya kiuchumi. 

Alisema baada ya Profesa Ndulu kupokea ombi hilo, alimpendekeza Dk Philip Mpango ambaye sasa ni Waziri wa Fedha na Mipango katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Kutokana na kuhitajika kwa kiasi kikubwa katika nchi yake, Gavana wa Benki Kuu wakati huo, Dk Daudi Balali alimwomba Kikwete amtafutie msaidizi na kiongozi huyo alimpendekeza Profesa Ndulu hivyo akawa Naibu Gavana BoT hadi Balali alipofariki dunia na kumwachia kiti Profesa Ndulu.

 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"