2/27/2021

SERIKALI IMETENGA MEGAWATI 70 ZA UMEME KUENDESHA TRENI YA MWENDOKASI, DKT. KALEMANI ASEMA HATA LEO TRENI IKIWA TAYARI UMEME UPO.

NA K-VIS BLOG, MOROGORO

WAZIRI wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani amesema Serikali kupitia TANESCO tayari imetenga Megawati 70 za umeme wa kuendesha treni ya mwendokasi maarufu SGR.

Mhe. Dkt. Kalemani ameyasema hayo leo Februari 27, 2021 wakati akifungua rasmi kikao kazi cha TANESCO na Wahariri wa vyombo vya habari kwenye ukumbi wa NSSF mkoani Morogoro.

Mahitaji halisi ya kuendesha treni hiyo ya umeme ni Megawati 27.

“Tunampongeza sana Rais wetu kwa kuamua kujenga SGR, hata treni hiyo ingekuwa tayari leo treni hiyo ingeendeshwa kwa umeme bila mashaka yoyote.” A.lisisitiza.

Alisema tayari miundombinu ya umeme kiasi cha kilomita 160 ikiwa ni pamoja na kuweka nguzo na nyaya za umeme kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro imekamilika na kwamba kinachosubiriwa ni kuiunganisha treni hiyo na umeme wa TANESCO.

Akizungumzia hali ya umeme nchini kwa sasa, Mhe. Waziri amewahakikishia watanzania na wawekezaji wa ndani na nje kuwa umeme wa kuhakikisha unaendesha uwekezaji wao upo wa kutosha na wa uhakika.

“Kwa sasa tuna jumla ya Megawati 1,604.28 za umeme huku mahitaji yetu ya umeme nchini kwa siku ni Megawati 1,180 na kwa maana nyingine tuna ziada ya umeme Megawati takriban 300.” Alifafanua Dkt. Kalemani.

Akizungumzia Mradi mkubwa wa Kimkakakti wa umeme wa maji wa Julius Nyerere (JNHPP2115), Mhe. Waziri alisema, ujenzi eneo la mradi unaendelea usiku na mchana chini ya usimamizi wa TANROADS na TANESCO.

Alisema mradi huo ambao unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali kwa thamani ya Shilingi Trilioni 6.5 ni wa kwanza kwa ukubwa katika nchi za Afrika Mashariki na wanne kwa ukumbwa barani Afrika, utaleta manufaa makubwa siyo tu ya kuzalisha umeme bali pia utunzaji wa mazingira, kilimo cha mseto, umwagiliaji na ufugaji.

“Kwa sasa watanzania tunatumia mkaa na kuni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, mathalan Dar es Salaam pekee kwa mwaka inatumia magunia msi chini ya magunia 400,000 hadi 500,000 kwa mwaka ambayo ni sawa na heka 1 ya miti.” Alifafanua.

Kwa hiyo umuhimu wa mradi huu utawawewezesha Watanzania kutumia nishati ya umeme kwa m atumizi ya nyumbani kwasababu mradi utakapokamilika gharama za umeme zitashuka sana, alibainisha Dkt. Kalemani.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtedaji wa TANESCO Dkt. Tito Mwinuka alisema madhumuni ya kikao kazi na wahariri wa vyombo vya habari ni kuwapa fursa ya kujenga uelewa wa shughuli mbalimbali za TANESCO hususan namna inavyotekeleza miradi mbalimbali kwa niaba ya Serikali ukiwemo mradi mkubwa w akimkakati w aumeme wa maji wa Julius Nyerere JNHPP2115.

“Lkani Pia tuna miradi kama vile Rusumo (MW 87) ambapo hadi sasa utekezwaji wake umefikia asilimia 76.8 na utagarimu kiasi cha shilingi billioni 263.

Hata hivyo Serikali kupitia TANESCO, inatarajia kutekeleza miradi mingine mikubwa kama vile Ruhuji 358 MW, Rumakali 222MW, Mtwara MW 300, Somanga fungu MW 300, Kakono MW 87, Malagarasi 45 MW.” Alisema Dkt. Kalemani.

Dkt. Mwinuka alisema Kupitia utekelezaji huu wa Miradi hii ya uzalishaji umeme, tunategemea hadi kufikia 2025 TANESCO kuwa na uwezo wakuzalisha Megawati 5,000. Hii itasidia Nchi kuwa na umeme wa kujitosheleza na utakaochochea ukuwaji wa uchumi na kuuza ziada itakayobakia nje ya Nchi.

Kwa upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abassi alisema “Nasimama hapa leo kuwapongeza sana TANESCO kwani ni miongoni mwa taasisi za umma zinazotekeleza wajibu wa kutoa habari kwa umma kikamilifu kwani ni haki ya kikatiba.

“Kila taasisi zinapaswa kutoa habari kwa kukutana na waandsihi wa habari kuwapeleka kwenye shughuli zao na miradi mbalimbali ili wananchi waweze kujua Serikali yao inavyowahudumia na tunakwenda kuzipima na kuzitathmini taasisi zote za umma ili kuja zinavyotekelza wajibu huu wa kikatiba.” Alisema.

Hata hivyo Dkt. Abbasi amewaasa waandishi kuzingatia misingi na kanuni za uandishi wa habari ili wajikite kwenye jukumu la msingi la kutoa habari kwa manufaa ya umma na kujiepusha na uandishi wa habari za kizandiki na uzushi.

"Silaha kuu ya mwandishi wa habari katika kutekelza majukumu yake ni kuandika ukweli na sio uzushi." Alifafanua.

WAZIRI wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani, akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi baina ya TANESCO na Wahariri wa vyombo vya habari kwenye ukumbi wa NSSF mjini Morogoro Februari 27, 2021

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abassi akitoa mada kuhusu wajibu wa vyombo vya habari 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Lowata Senare akizungumza kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka akitoa maelezo kuhusu utekelzaji wa miradi ya shirika
Bi. Joyce Shebe, mwakilishi wa Wahariri akizungumza
Baadhi ya watendaji wa TANESCO
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO, Bw.Rodney Thadeus (katikati) akifuatilia kikao kinavyoendelea

Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Johary Kachwamba (kushoto) na Afisa Uhusiano Mwnadamizi wa shirika hilo, Bi. Grace Kisyombe.





Baadhi ya wahariri wakiwa kwenye kikao hicho.
Baadhi ya wahariri wakiwa kwenye kikao hicho.


Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (kushoto) na Mkurugenzi Mtendajiw a TANESCO Dkt. Tito Mwinuka wakiwa kwenye kikao.

    

0 comments:

Post a Comment