1/27/2021

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AZINDUA SHAMBA LA MITI CHATO MKOANI GEITA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimwagilia maji mti alioupanda kama kumbukumbu mara baada ya kuzindua shamba la Miti lenye ekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, Waziri wa Madini Doto Biteko, Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu TFS Profesa Dos Santos Silayo   pamoja na viongozi wengine akizindua shamba la Miti lenye ukubwa wa ekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Butengo Chato mkoani Geita kabla ya kuzindua Shamba kubwa la Miti lenye jumla ya ekari elfu 69 mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.

Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu TFS Profesa Dos Santos Silayo akipiga Saluti mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kutangaza Rasmi kuwa Shamba la Miti la Chato sasa liitwe Shamba la Silayo kama Heshima kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi. (PICHA NA IKULU).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Uyovu mkoani Geita wakati akielekea Kahama mkoani Shinyanga leo tarehe 27 Januari 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Butengo Chato wakati akiondoka katika shamba la Miti la Chato mara baada ya kulizindua mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
 

    

0 comments:

Post a Comment