12/03/2020

POLISI SHINYANGA WADAU WAADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

 

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizindua Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amezindua Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanaopinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yakiongozwa na Kauli mbiu 'Tupinge Ukatili wa kijinsia, Mabadiliko yanaanza na mimi'. 

Akifungua maadhimisho hayo leo Jumatano Disemba 2,2020 katika Viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga,Kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mboneko amesema ni wajibu wa kila mtu katika jamii kushiriki kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake, wanaume na watoto. 

“Ukatili wa kijinsia ni uhalifu kama ulivyo uhalifu mwingine, ni lazima kila mmoja ashiriki katika kuutokomeza kwani ukatili unapotokea katika jamii wanaoathirika zaidi ni wanawake na watoto”,amesema Mboneko. 

“Chapa kazi siyo kuchapa mke, mme au mtoto. Lakini pindi matukio ya ukatili ikiwemo ubakaji, mimba na ndoa za utotoni yanapotokea toeni taarifa kwenye vyombo vinavyohusika ili hatua zichukuliwe haraka kwani tunataka watu wote wawe salama”,ameongeza Mboneko. 

Katika hatua nyingine amewataka viongozi wa serikali kuanzia wa serikali za mitaa kusimamia ipasavyo haki za binadamu kwa kutoyafumbia macho matukio ya ukatili bali wachukue hatua haraka.

Mboneko amewashauri wawazi na walezi kutenga muda kwa ajili ya kukaa na watoto ili kubaini changamoto zinazowakabili lakini pia kuwaeleza madhara ya ukatili wa kijinsia. 

Mkuu huyo wa wilaya pia ametumia fursa hiyo kuwataka wanaume wanaofanyiwa vitendo vya ukatili ikiwemo kupigwa na wake zao watoe taarifa kwenye mamlaka husika yakiwemo madawati ya Jinsia na Watoto. 

Pia amewataka wadau mbalimbali kuendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia akisisitiza umuhimu wa kutumia wasanii wa nyimbo za asili kufikisha elimu katika jamii. 

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba amesema jeshi la polisi kupitia Mtandao wa Wanawake Polisi na Dawati la Jinsia na Watoto wanaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia. 

Kamanda Magiligimba amesema hivi sasa kuna mwamko mkubwa wa jamii kuripoti matukio ya ukatili wa kijinsia akitolea mfano kuwa katika kipindi cha mwezi Juni hadi Agosti 2020 kumeripotiwa matukio 231 ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ikilinganishwa na kipindi cha Mwezi Juni hadi Agosti mwaka 2019 ambapo kulikuwa na matukio 151 ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

“Tunashukuru wananchi wameanza kuziamini ofisi za madawati ya jinsia takribani matano tuliyonayo katika mkoa wa Shinyanga ambapo wamekuwa wakitoa taarifa za matukio ya ukatili wa kijinsia. Lakini pia tunazishukuru taasisi na mashirika tunayoshirikiana nayo katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia”,amesema. 

Kamanda Magiligimba ametumia fursa kuwataka wazazi na walezi kuachana na tabia ya kuwalaza watoto kwenye chumba kimoja na wageni wanaofika nyumbani kwani baadhi yao siyo watu wema wamekuwa wakiwafanyia vitendo vya ukatili watoto. 

“Matukio mengi ya ukatili katika na watu wetu wa karibu,ndugu zetu. Usikubali mgeni alale chumbani na mtoto wako. Usilaze mtoto chumba kimoja na mgeni kwani baadhi yao wanawafanyia ukatili ikiwemo kuwabaka na kuwalawiti watoto”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

“Naomba pia wazazi na walezi waache kumaliza kesi za matukio ya ukatili wa kijinsia kifamilia. Mzazi usikae na kusuluhisha kesi ya mtoto kufanyiwa ukatili,toa taarifa ili watuhumiwa wachukuliwe hatua za kisheria ili kutokomeza matukio ya ukatili wa kijinsia”,ameongeza. 

Aidha Kamanda huyo amezitaka familia kuacha kuficha matukio ya ukatili wa kijinsia na kulipana fidia watoto wakifanyiwa ukatili ili kumaliza kesi na kuhakikisha wanatoa ushahidi kuhusu matukio hayo sambamba na kuepuka kutoa ushahidi wa uongo hali ambayo inakwamisha kesi za matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

 ANGALIA PICHA HAPA CHINI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifungua Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack leo Jumatano Disemba 2,2020 katika Viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga. Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yameandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali yakiongozwa na Kauli Mbiu ya 'Tupinge Ukatili wa Kijinsia,Mabadiliko yanaanza na mimi" - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifungua Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack leo Jumatano Disemba 2,2020 katika Viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga. Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yameandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifungua Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack leo Jumatano Disemba 2,2020 katika Viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga. Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yameandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Luther Mneney akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Mwakilishi wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT) mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, ACP Africanus Sulle akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Mkuu wa Dawati la Jinsia la Watoto mkoa wa Shinyanga , Victoria Maro akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Meza kuu wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea.
Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Shinyanga SP Davis Msangi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Uhuru Edward Kulwa akiimba shairi wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Vijana kutoka kikundi cha burudani cha Kambi ya Nyani wakitoa burudani
Kwaya ya AIC Shinyanga ikitoa burudani.
Burudani ikiendelea 
Burudani ikiendelea
Wanafunzi wa shule ya sekondari Uhuru wakionesha igizo
Meza kuu wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Meza kuu wakifuatilia burudani kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wanafunzi wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wanafunzi wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wanafunzi wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
Wadau wakiwa kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia
    

0 comments:

Post a Comment