RC KUNENGE AWAHAKIKISHIA WANANCHI USALAMA SIKU YA UCHAGUZI, ASEMA YOYOTE ATAKAEFANYA FUJO ATAKIONA CHA MOTO


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge ametoa onyo kali kwa watu au vikundi vya watu vilivyopanga kufanya fujo siku ya uchaguzi ambapo ameeleza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga vizuri kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na usalama.

RC Kunenge ametoa onyo hilo wakati alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari ambapo ametoa wito kwa wananchi wote waliojiandikisha kutumia haki yao ya msingi kwa kutijokeza kwa wingi kwenye vituo vya kupigia kura ili waweze kuchagua viongozi wanaowataka.

Aidha RC Kunenge ameeleza kuwa hali ya amani na utulivu kwenye jiji hilo ni shwari na utaendelea kuwa shwari siku zote hivyo hakuna sababu yoyote ya wananchi kuwa na wasiwasi.

Uchaguzi Mkuu wa viongozi wa ngazi ya Urais, Wabunge na Madiwani utafanyika October 28 ambapo Rais Dkt. John Magufuli amepanga siku hiyo kuwa ya mapumziko ili kila mwananchi aweze kupata nafasi ya kutumia haki yake ya msingi ya kupiga kura.

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"