KUSAYA AKARIBISHA WAWEKEZAJI KUZALISHA MBEGU ZA MAZAO YA KILIMO.
Mwonekano wa mradi wa ujenzi wa vihenge vya kisasa 6 vyenye uwezo wa kuhifadhi nafaka tani 20,000 katika kituo cha NFRA Songwe. Mradi huo unatarajia kukamilika Desmba mwaka huu ukigharimu dola za kimarekani milioni 5.2 .Kukamilika kwa mradi huu kutaongea uwezo wa kituo kuhifadhi tani 37,000 za nafaka.
WIZARA
YAKARIBISHA WAWEKEZAJI KUZALISHA MBEGU ZA MAZAO KILIMO
WIZARA
ya Kilimo imetoa wito kwa wawekezaji wa ndani ya nchi kushirikiana na Wakala wa
Mbegu (ASA) kuzalisha mbegu bora nyingi na zenye tija na kuwezesha wakulima
kupata kwa gharama nafuu.
Wito
huo umetolewa jana (19.10.2020) na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya
alipotembelea na kukagua utendaji kazi wa shamba la Mbegu la ASA Mbozi mkoani
Songwe.
“Nakaribisha
wawekezaji katiuka uzalishaji mbegu lakini lengo la wizara ni kupata mbegu bora
ambazo zitamfikia mkulima kwa gharama nafuu na kwa wakati “alisema Kusaya.
Kusaya
ambaye aliambatana kwenye ziara hiyo pamoja na makampuni yanayojihusisha na
uzalishaji mbegu pamoja na ASA ikiwemo Jeshi la Kujenga Taifa aliwataka kuendelea kutumia ardhi kubwa
iliyopo kuzalisha mbegu bora zinazohitajika na wakulima wa Tanzania na
kupunguza utegemezi wa nje.
“Natoa
rai kwa Jeshi la KLujenga Taifa njooni hapa Mbozi mshirikiane na wakala wetu
ASA mzalishe mbegu bora ili ushirikano wetu usaidie Taifa kuwa na mbegu bora
zilizotafitiwa na watanzania wenyewe badala ya mbegu za kutoka nje ya nchi”
alisisitiza Kusaya
Akitoa
taarifa ya hali ya upatikanaji mbegu za mazao nchini, Mtendaji Mkuu wa ASA Dkt.
Sophia Kashenge alisema wakala huo unayo mashamba 10 yanayozalisha mbegu
takribani asilimia 21 hdi 25 inayotumika nchini.
Dkt.
Sophia aliongeza kusema katika mwaka 2020/21 wakala kwa ushirikiano na
makampuni binafsi na taasisi za umma umeweza kuzalisha mbegu mbalimbali za
mazao tani 5,600
Kuhusu
uzalishaji wa mbegu bora za michikichi aina ya Tenera zenye kutoa mavuno
mengi,Dkt. Sophia alisema ASA tayari imefanikiwa kuzalisha miche 342,000
katikam vituo vyake vitatu ambayo itagawiwa kwa wakulima wa Kigoma,Morogoro na
Mbozi.
Katibu
Mkuu Kilimo alipongeza ASA kwa kuzalisha miche bora ya michikichi 42,000 katika
shamba lake la Mbozi hali itakayosaidia kuongeza wigo wa uzalishaji michikichi
kama livyoagizwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Kusaya
alisema Tanzania kwa sasa inatumia zaidi ya Shilingi Bilioni 443 kwa ajili ya kuagiza
mafuta ya kula nje ya nchi hivyo lengo
la seriklai kuhamasisha kilimo cha michikichi ili nchi ijitosheleze kwa mafuta.
Katika
hatua nyingine Katibu Mkuu huyo alitembelea Kituo cha Utafiti wa kahawa (TACRI)
Mbimba wilayani Mbozi na kufahamishwa kuwa kituo hicho kimefanikiwa kuzalisha
na kusambaza miche bora ya kahawa milioni 11.2 kwa wakulima wa mikoa ya Songwe,
Mbeya,Rukwa na Katavi katika kipindi cha mwaka 2008 hadi 2020.
Akitoa
taarifa ya kituo hicho Meneja wa TACRI Mbimba Isaack Mushi aliongeza kusema
kituo kimefanikiwa pia kuwafikia wakulima 74,565 katika wilaya 10 za Nyanda za
Juu Kusini na kuwapa elimu ya kilimo bora cha kahawa.
“Msimu
wa 2020/21 tunatarajia kuzalisha na kusambaza miche bora ya kahawa milioni 4.5
kwa wakulima hali itakayokuza uzalishaji kahawa” alisema Mushi.
Kuhusu
takwimu za unywaji kahawa Mushi alisema watanzania wanakunywa kahawa asilimia 7
tu ya kahawa yote inayozalishwa nchini hali inayopunguza upatikanaji wa soko.
Katibu
Mkuu Kusaya alitoa agizo kwa watafiti wa zao la kahawa kuongeza bidii ya
kuwezesha miche mingi ya kahawa iwafikie wakulima na kukuza uzalishaji wa zao
hilo ambalo linaingiza fedha nyingi nchini.
Kusaya
alisisitiza umuhimu wa mbegu bora za kahawa na kusema” tunahitaji mbegu bora
nyingi himilivu kwa magonjwa na zenye kuongeza tija kwa mkulima katika
mazingira yake “na kuongeza kuwa watafiti wanalo jukumu la kuwezesha ubora wa
kahawa inayozalishwa Tanzania kuwa na soko
la uhakika.
Katika
hatua nyingine akiwa mkoani Songwe, Kusaya alikagua
mwenendo wa ununuzi wa mahindi katika kituo cha wakala wa Taifa wa Chakula
(NFRA) Songwe na kuelezwa kuwa tayari tani 9,191 za mahindi kati ya lengo la
tani 30,000 msimu wa 2020/21 zimenunuliwa toka kwa wakulima kwa bei ya wastani
ya shilingi 550.
Taarifa
hiyo iliyotolewa na Kaimu Meneja wa NFRA kanda ya Songwe Eva Kwavava ilisema
kituo hicho kina uwezo wa kuhifadhi tani 17,000 za nafaka na mpaka mwezi Octoba
mwaka huu kina nafaka tani 10,483 zilizohifadhiwa kwenye maghala yake.
Kusaya
alikagua pia mradi wa ujenzi wa vihenge vya kisasa 6 vyenye uwezo wa tani
20,000 vinavyojengwa na mkandarasi M/S Feerum S.A ya Poland na kusimamiwa na
Wakala wa Majengo (TBA) ambayo vinatarajia kukamilika Desemba 2020 kwa gharama
dola za kimarekani milioni 5.2
Wakala
wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula katika msimu unaoendelea wa ununuzi tayari
umenunua tani 110,000 kati ya lengo la tani 300,000 kwa gharama ya Shilingi
Bilioni 15 zilizotolewa na serikali katika kanda zake nane nchini.
Katibu
Mkuu Kusaya leo anaendelea na ziara yake mkoani Rukwa kwa kutembelea taasisi
chini ya wizara na kuzungumza na watumishi wa sekta hiyo.
Comments
Post a Comment