NA MWANDISHI WETU, RUKWA
MKUU wa mkoa wa
Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi 638,979 wa vijiji vyote 339, Mitaa
167, Kata 96, Tarafa 16, Halmashauri 4 na Wilaya 3 Mkoani Rukwa walioandikishwa
kwaajili ya kupiga kura, kujitokeza katika kupiga kura katika uchaguzi mkuu
utaofanyika siku ya Jumatano ya tarehe 28 mwezi Oktoba mwaka huu ili kuwachagua
Madiwani, Wabunge Pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, Mh. Wangabo ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha wakulima
kuwa katika kipindi hiki cha Kampeni wasisahau kuandaa mashamba yao kwaajili ya
msimu wa kilimo wa mwaka 2020/2021 na kusisitiza kuwa wananchi wasiegemee sana
siasa wakasahau Maisha ya kawaida ambayo ni kilimo kwa wananchi wengi wa mkoa
wa Rukwa.
“Wakati huo huo vyote lazima viende Pamoja na maandalizi ya
kilimo, si mvua karibu zinanyesha, ni lazima watu wakaandae mashamba yao,
tusiegemee sana siasa tukasahau pia kuna Maisha ya kawaida kwetu sisi ni
kilimo, kwahiyo ni lazima tuandae mashamba mapema, uchaguzi unapopita mvua
zikinyesha tunakwenda kupanda, mvua za kwanza ni za kupandia, kwahiyo vyote
tuvibebe, tumeelewana,” Alisistiza.
Mh. Wangabo ameyasema hayo leo tarehe 22.9.2020. alipotembelea
miradi ya Lipa kulingana na Matokeo (EP4R) na Miradi ya Afya na Usafi wa
Mazingira (SWASH) inayotekeleza ujenzi wa madarasa na vyoo vya wananfunzi kwa
shule za msingi na Sekondari Wilayani Kalambo ambapo wilaya hiyo imepokea jumla
ya Shilingi 529,679,504 kwa mwaka huu wa fedha ili kutekeleza miradi hiyo.
Awali wakati akisoma taarifa ya miradi hiyo kwa niaba ya
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, Afisa Mipango wa Halmashauri
hiyo Eric Kayombo alisema kuwa Shilingi 353,900,000 ilipokelewa katika shule
saba za msingi kwaajili ya ujenzi wa madarasa na vyoo na Shilingi 175,776,504
ilipokelewa katika shule nyingine 7 za msingi kwaajili ya ujenzi wa vyoo.
“Mheshimiwa Mkuu wa mkoa utekelezaji wa miradi hii umeanza mwaka
huu wa fedha 2020/2021 badala yam waka 2019/2020 hii ni kutokana na halmashauri
kupokea fedha za miradi mwishoni mwa mwaka wa fedha 2019/2020 na kufanya kuvuka
mwaka na kuanza kutekeleza mwaka huu wa fedha, Miradi ya EP4R ipo katika hatua
za msingi na miradi ya afya na usafi wa mazingira ipo katika hatua mbalimbali
za utekelezaji,” Alisema.
Mh. Wangabo ametoa miezi miwili kwa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kuhakikisha wanamaliza miradi hiyo kwa shule za msingi na sekondari ili kuimarisha miundombinu ya shule hizo ambazo iradi hiyo inatekelezwa ikiwemo shule ya sekondari ya Wasichana Matai ambayo inatarajiwa kuanza kupokea wananfunzi kuanzia mwaka 2021.
Mkuu wa Mkoa wa
Rukwa Mh. Joachim Wangabo akikagua ujenzi wa vyoo vya wananfunzi vinavyojengwa
kwa fedha za mradi wa Afya na Usafi wa Mazingira (SWASH) katika shule ya Msingi
Kafukoka, Kata ya Samazi, Wilayani Kalambo
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Mh. Joachim Wangabo pamojana uongozi wa Wilaya ya Kalambo walipotembelea
kukagua ujenzi wa vyoo vya Shule ya Msingi Ngorozwa, Kata ya Kasanga, Wilayani
Kalambo vinavyojengwa kwa mradi wa Lipa kulingana na Matokeo (EP4R).
Mkuu wa Mkoa wa
Rukwa Mh. Joachim Wangabo akikagua ujenzi wa shimo la vyoo vya wananfunzi
vinavyojengwa kwa fedha za mradi wa Afya na Usafi wa Mazingira (SWASH) katika
shule ya Msingi Kafukoka, Kata ya Samazi, Wilayani Kalambo
0 comments:
Post a Comment