BAADA YA KENYA KUKUBALI "YAISHE" TANZANIA NAYO YARUHUSU NDEGE ZA KENYA KUTUA NCHINI
HATIMAYE serikali ya Kenya imeiorodhesha Tanzania kati ya nchi ambazo raia wake wanaruhusiwa kuingia nchini humo bila kulazimishwa kuwekwa karantini ya siku 14 kutokana na maambukizi ya virusi vya Corona.
Uamuzi huo wa Serikali ya Kenya ulitangazwa Septemba 15, 2020 katika taarifa iliyotolewa na Mkuu wa idara ya uhamiaji nchini Kenya Alexender Muteshi ambapo Tanzania iko kwenye namba 132.
Awali Kenya ambayo ni Mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania, Burundi, Rwanda, Uganda na Sudani Kusini ilitoa orodha ya mataifa ambayo raia wake hawalazimiki kukaa karantini ya siku 14 waingiapo nchini humo lakini Tanzania na Burundi hazikuwekwa kwenye orodha hiyo, hali iliyozusha hasira kutoka Tanzania ambayo nayo kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) ikatoa taarifa ya kufuta kibali cha ndege za Kenya kutua nchini Tanzania.
Comments
Post a Comment