HESLB YAONGEZA MUDA WA KUPOKEA MAOMBI YA MIKOPO YA WANAFUNZI ELIMU YA JUU
ISMAIL
NGAYONGA, DAR ES SALAAM
BODI
ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeamua kuongeza muda wa kupokea
maombi ya mikopo kutoka kwa wanafunzi hadi Septemba 10, 2020 mwaka huu, Mkurugenzi
Mtendaji Abdul-Razaq Badru amesema.
Bw.
Badru ameyasema hayo wakati akitoa taarifa kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya
Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe leo (Jumatatu, Agosti 31, 2020) amefalipofika
kwenye ofisi za Bodi hiyo jijini Dar es Salaam kwa nia ya kujionea utendaji
kazi wa Bodi.
“Tunaendelea
vizuri na majukumu yetu na kutokana na kupokea maoni mengi ya wadau, HESLB imeamua
kuongeza muda wa kupokea maombi ya mikopo kutoka kwa wanafunzi hadi Septemba 10
mwaka huu.” Alisema.
Bw.
Abdul-Razak Badru alisema “Mwisho ilikua
iwe leo saa sita usiku, lakini tumeamua kuongeza siku kumi ili kuwawezesha
wateja wetu ambao hawajakamilisha maombi yao kufanya hivyo,” amesema Badru na
kuongeza kuwa uamuzi huo umefuatia mashauriano na wadau wengine kama Wakala wa
Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) na Shirika la Posta Tanzania (TPC) ambazo
nazo zinawahudumia wateja hao.
Kuhusu
malipo kwa wanafunzi waliopo vyuoni, Badru amesema TZS 15.57 bilioni zimetumwa
vyuoni kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi wanufaika 39,721 kuendelea na mafunzo
kwa vitendo katika maeneo mbalimbali kuanzia wiki hii.
Kwa upande wake, Prof. Mdoe aliieleza Menejimenti hiyo ya HESLB chini ya Mkurugenzi Mtendaji Abdul-Razaq Badru kuwa waendelee kuchapa kazi.
“Nimekuja
kuona mmejiandaaje na mwaka mpya wa masomo na hali ya uombaji mikopo
inavyoendelea na nimefurahi kusikia mnaendelea vizuri, endeleeni kuchapa kazi,”
amesema Prof. Mdoe katika kikao kazi na wajumbe wa menejimenti ya HESLB
kilichofanyika katika ofisi za HESLB zilizopo eneo la TAZARA.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimuya Juu (HESLB) Abdul-Razaq
Badru (kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,
Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe wakati alipofanya ziara katika Ofisi za
HESLB na kuzungumza na menejimenti ya HESLB iliyoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji
leo Jumatatu (Agosti 31, 2020) Jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment